Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa daraja la juu katika Mto Mwamanongu?

Supplementary Question 1

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru hadi hapo ilipofikia ni kazi kubwa imefanywa na Serikali, Mheshimiwa Rais Samia alipita njia hiyo akaiona hiyo adha kwenye hilo daraja. Je, Serikali iko tayari kutoa kipaumbele kwenye mwaka ujao wa fedha kwa sababu Wilaya tumetenga hizo fedha? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mvua inaponyesha Kata ya Mwabuzo, Mwamanongu, Imaraseko, Mwamalole hukata mawasiliano na Wilaya. Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kuja kuiona hiyo adha wanayopata Wananchi wa Jimbo la Meatu? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali ipo tayari kutoa kipaumbele kwa ajili ya ujenzi wa daraja hili ambalo Mheshimiwa Mbunge aliliuliza kwenye swali lake la msingi na tutaangalia kadri ya upatikanaji wa fedha kwenye mwaka wa fedha 2023/2024, kuona ni namna gani tunaweza kuanza na kama fedha basi zitakuwa hazitoshi katika mwaka huo wa fedha tutaenda kuona tunatenga fedha kwa ajili ya kutekeleza pia ahadi hii ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mwaka wa fedha 2024/2025.

Mheshimiwa Spika, nikijibu swali lake la pili la kama nipo tayari kuongozana naye kwenda kuona namna miundombinu ilivyoharibika katika maeneo haya ya Jimbo lake kule Meatu. Nipo tayari kuongozana nae na baada tu tukihitimisha Bunge hili la bajeti tarehe 30 Juni mwaka huu, mimi nipo tayari kupanga na Mheshimiwa Komanya ili tuweze kuelekea wote kule Meatu.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa daraja la juu katika Mto Mwamanongu?

Supplementary Question 2

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante, Kata ya Mwamishali ina changamoto ya daraja la kutoka Mwambiti, Tongoleangamba hadi Buliashi ambayo ni Makao Makuu.

Je, ni lini Serikali itajenga daraja hilo? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali itajenga daraja hili la Mwamishali kuelekea Makao Makuu ya Kata kadri ya upatikanaji wa fedha. Tutaangalia katika mwaka huu wa fedha 2023/2024 kuona kama fedha imetengwa kwa ajili ya usanifu na ujenzi wa daraja hili na kama haijatengwa tutatenga katika mwaka wa fedha wa 2024/2025 kadri ya upatikanaji wa fedha hizo.