Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdulhafar Idrissa Juma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtoni

Primary Question

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA aliuliza:- Je, kuna mpango gani wa kusaidia upatikanaji wa Bima ya Afya kwa watoto wasio na wazazi ambao walikuwa wakilipiwa bima na wahisani?

Supplementary Question 1

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA: Mheshimiwa Spika nashukuru, nina swali moja la nyongeza.

Je, Serikali imeshapeleka elimu kwa Wakuu wa Shule na Kamati za Shule hasa shule za Serikali zilizoko vijijini kwamba ipo huduma hii ya afya kwa watoto na inaweza kupatikana kupitia shule? Nashukuru. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, anasema kama Serikali imeshapeleka. Ni kweli tumeshaanza kupeleka na kwa sababu suala la elimu ni endelevu, tunaendelea kupeleka, lakini pia nilitumie Bunge lako tukufu, nawaomba Wabunge kwenye mikutano yetu ya kwenye Wilaya zetu, tuendelee kuwasisitiza wananchi na watu wengine na Serikali ya Wilaya na watu wengine kuhakikisha wanahamasisha hili na kuwapa taarifa wazazi, tufanye hilo kwa pamoja.

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA aliuliza:- Je, kuna mpango gani wa kusaidia upatikanaji wa Bima ya Afya kwa watoto wasio na wazazi ambao walikuwa wakilipiwa bima na wahisani?

Supplementary Question 2

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, wakati tunasubiri mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, Serikali inatumia utaratibu gani kuwapatia matibabu watu wenye ulemavu wasiokuwa na uwezo? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kuna utaratibu wa kutoa matibabu bure kwa watu wasio na uwezo wa kujilipia. Kwenye eneo lake la kata yake, akishapata barua ya Katibu Kata akienda hospitali na kuna watu wa Maendeleo ya Jamii kwenye kila hospitali yetu, ambao wanashughulikia mambo hayo na wanaweza kumsaidia na akapata huduma bure kama hana uwezo wa kujilipia.