Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 9 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 137 2023-09-08

Name

Abdulhafar Idrissa Juma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtoni

Primary Question

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA aliuliza:-

Je, kuna mpango gani wa kusaidia upatikanaji wa Bima ya Afya kwa watoto wasio na wazazi ambao walikuwa wakilipiwa bima na wahisani?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdul-Hafar Idrissa Juma, Mbunge wa Mtoni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa mfumo wa kulipia watoto kupitia Toto Afya Kadi umebadilika na kwa sasa unafanyika kupitia utaratibu wa shule na vifurushi vya bima ya afya vya najali, wekeza na Timiza.

Mheshimiwa Spika, suluhisho la kudumu la tatizo hili, ni kukamilika kwa Muswada wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ambao tunaamini utawezesha watoto wengi zaidi wasio na changamoto ya kiafya na wenye changamoto za kiafya kulipiwa Toto Afya Kadi. Hatua hii itasababisha kuwepo kwa uhai na uendelevu wa Mfuko wa Bima ya Afya, naomba kuwasilisha.