Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Je, lini Serikali itaviendeleza viwanda vya nyama na samaki Mkoani Rukwa?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa Mkoa wa Rukwa ukepakana na maziwa mawili likiwemo Ziwa Tanganyika na Ziwa Rukwa. Serikali ina mpango gani wa kuanzisha uvuvi wa vizimba katika maziwa hayo, ili kupata malighafi ya samaki kwa wingi?

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili; nilitaka kujua Serikali ina mpango gani wa kukiendeleza Kiwanda cha SAAFI kilichopo Mkoa wa Rukwa ambacho kilianzishwa na Hayati Chrisant Mzindakaya? Ahsante.

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, kwanza nimshukuru na kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa kutambua umuhimu wa ufugaji wa samaki kwa njia ya kisasa, kwa maana ya vizimba katika Maziwa ya Rukwa na Tanganyika.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi tayari imeshaanza zoezi hilo. Tumeanza katika Mkoa wa Mwanza kwa maana ya Ziwa Victoria, tayari tunafuga kupitia vizimba. Kwa hiyo, nitoe wito kwa wataalamu wetu waweze kutembelea kwenye maziwa haya kwa kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge, ili waweze kuanzisha ufugaji wa samaki kupitia vizimba katika Ziwa Rukwa na Ziwa Tanganyika na ninakuomba Mheshimiwa Mbunge uweze pia, kushirkiana nasi ili uweze kuwa kinara katika ufugaji huu wa kisasa wa samaki.

Mheshimiwa Spika, pili; kuhusiana na kiwanda hiki cha Sumbawanga Agricultural and Animal Food Industries Limited kwa maana ya SAAFI, changamoto kubwa ilikuwa ni fedha na uendeshaji wa kiwanda hiki ambacho ni kiwanda cha kisasa sana hapa nchini. Serikali tayari imeshaanza kupitia Benki ya Uwekezaji Tanzania (TIDB), kutafuta mwekezaji mpya baada ya changamoto zilizokuwepo kwa mwekezaji yule wa mwanzo.

Kwa hiyo, tumeshatangaza tayari kupitia gazeti mwezi wa Agosti, kupata mwekezaji mpya ili aweze kuingia ubia na waliopo ili kuhakikisha kiwanda hiki kinafufuliwa, nakushukuru.

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Je, lini Serikali itaviendeleza viwanda vya nyama na samaki Mkoani Rukwa?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER E. MALEKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, katika kutekeleza Sera ya Tanzania ya Viwanda, nini mkakati wa Serikali kufufua viwanda vilivyopo katika Mkoa wa Kilimanjaro ili kuwapatia wananchi wetu ajira, lakini pia kuongeza uchumi wa Mkoa wetu wa Kilimanjaro? Ahsante.

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kama nilivyosema nia ya Serikali ni kuhakikisha tunaendelea kutekeleza sera ya kuwa nchi ya viwanda na kama tulivyosema tuwe na uchumi unaoendeshwa na viwanda hapa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, tumeendelea kutafuta wawekezaji kwa sababu, tunaondokana na uchumi hodhi, kwa maana ya Serikali kufanya biashara au kuendesha viwanda. Kwa hiyo, Mkoa wa Kilimanjaro na Mikoa mingine ambako kuna viwanda vyenye changamoto, vile ambavyo vitakuwa vimebinafsishwa, lakini havijaendelezwa au vingine ambavyo tunaona havifanyi kazi, tutaendelea kutafuta wawekezaji kwa kuweka kwenye masharti nafuu, pia vivutio mbalimbali ili kuvutia uwekezaji wa ndani, hata wawekezaji kutoka nje ili kuhakikisha viwanda hivyo vimefanya kazi na kupunguza nakisi ya bidhaa mbalimbali ambazo zinatumika nchini kuagizwa nje, lakini pia kutoa masoko kwa malighafi ambazo zinatumika kwenye viwanda hivyo ambavyo vinzalishwa hapa nchini, nakushukuru.