Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 9 Industries and Trade Wizara ya Viwanda na Biashara 134 2023-09-08

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:-

Je, lini Serikali itaviendeleza viwanda vya nyama na samaki Mkoani Rukwa?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, uendelezaji wa sekta ya viwanda ikiwemo viwanda vya nyama na samaki katika Mkoa wa Rukwa na mikoa mingine nchini ni endelevu. Serikali inaendelea na juhudi za kuhamasisha uwekezaji wa viwanda vipya na uendelezaji wa viwanda vilivyopo katika sekta ya mifugo na uvuvi hususani viwanda vya kuchakata mazao ya mifugo na uvuvi.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto ya upatikanaji wa malighafi ya mazao ya mifugo na uvuvi inayovikabili viwanda vya nyama na samaki katika Mkoa wa Rukwa na mikoa mingine nchini. Kwa sasa Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeweka nguvu kubwa katika unenepeshaji wa mifugo pamoja na ufugaji wa samaki kwa kutumia vizimba, kutenga na kuboresha maeneo ya ukusanyaji samaki (collection centers) pamoja na minada ya mifugo ili kukidhi haja ya upatikanaji endelevu wa malighafi bora ya viwanda vya nyama na samaki nchini ikiwemo katika Mkoa wa Rukwa.

Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali inaendelea na juhudi za kukabiliana na tatizo la utoroshaji wa mazao ya samaki na mifugo kwenda nchi za jirani bila kufuata taratibu ili kukidhi mahitaji ya malighafi katika viwanda vyetu vya ndani. Hivyo, nitoe rai kwa wavuvi na wafugaji kuviuzia malighafi viwanda vyetu vya ndani ili viweze kukidhi mahitaji yake, nakushukuru.