Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Njia Panda - Mangola - Matala hadi Lalago kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi; barabara ya Bungu kuelekea Kibirizi ambayo inamilikiwa na TANROADS hali yake ni mbaya sana na haipitiki kwa sasa. Je, mna mpango gani wa kukarabati barabara hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, bahati nzuri barabara hiyo naifahamu sana, siyo barabara ndefu ni barabara ambayo ipo katikati ya Mji. Naomba nitumie nafasi hii kumuagiza Meneja wa TANROADS aipitie hiyo barabara na iweze kukarabatiwa kwa sababu imetengewa fedha kwenye matengenezo ya kawaida. Kwa hiyo, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge barabara hiyo itakarabatiwa katika kipindi hiki cha mwaka wa fedha.

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Njia Panda - Mangola - Matala hadi Lalago kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza Serikali Bunge lililopita iliahidi kujenga na kusaini barabara ya Bigwa – Kisaki hadi sasa ipo kimya; je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Bigwa – Kisaki?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, barabara hiyo imeshapata mkandarasi na sasa hivi kinachoandaliwa tu ni taratibu za kuisaini hiyo barabara. Kwa hiyo tuna barabara kama 16 ambazo zinaandaliwa utaratibu mzuri wa kuzisaini ili Wakandarasi waanze kazi, ikiwepo na hiyo barabara ya Bigwa – Kisaki.

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Njia Panda - Mangola - Matala hadi Lalago kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa barabara hii imeahidiwa toka Serikali ya Awamu ya Nne na iko kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi.

Je, ni lini Serikali sasa itatenga angalau kwa kilomita chache ili kuwezesha wananchi wale wa Bonde la Eyasi kuweza kusafirisha mazao yao kwenda kwenye masoko ya nchi ya jirani? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba barabara aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge ipo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi na tunatambua kwamba barabara hii ni muhimu sana. Kama nilivyosema katika jibu la msingi, barabara hii ilitakiwa ijengwe lakini imejengwa barabara ambayo ni Serengeti Southern Bypass.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali inachofikiria kufanya ni kujenga walau kilometa 50 ambazo zitaanzia pale Njia Panda hadi eneo la Mang’ola ambalo lina uzalishaji mkubwa sana na hasa zao la vitunguu. Kwa hiyo, Serikali sasa inafikiria kulifanya halafu baadae ndiyo ije kukamilisha kipande kilichobaki ambacho kinapita sehemu kubwa ya mbuga, ahsante.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Njia Panda - Mangola - Matala hadi Lalago kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, hali ya Daraja la Mto Ubagwe hali ni mbaya sana na Mheshimiwa Waziri ni shahidi alituma watu wa TANROADS.

Ni lini Serikali inaanza ujenzi wa daraja hili ili kuwanusuru wananchi na hali ya mvua?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunafahamu na tumefanya mawasiliano makubwa, nimtoe shaka naamini daraja hilo ambalo ni muhimu sana kwa Wilaya ya Ushetu litaanza kujengwa kipindi hiki cha mwaka huu wa fedha, ahsante.

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Njia Panda - Mangola - Matala hadi Lalago kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, pamoja na kutengewa fedha kwenye bajeti, bado hakuna hatua yoyote ambayo imeanza mpaka sasa.

Ni lini Serikali itaanza taratibu za ujenzi wa barabara ya lami ya kutoka Korogwe – Dindila – Soni mpaka Bumbuli? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, barabara hii anayoitaja Mheshimiwa Mbunge tumeitengea bajeti, kwa maana ya utekelezaji wa mwaka huu wa fedha, tayari tender documents zinaendelea kuandaliwa ili barabara hiyo iweze kutangazwa kwa ajili ya kuanza ujenzi. (Makofi)

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Njia Panda - Mangola - Matala hadi Lalago kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. STANSALAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Spika, kutokana na jibu la swali la msingi, kwamba tayari barabara hii imeshasainiwa mkataba. Naomba kuiuliza Serikali baada ya kusaini mkataba ni muda gani Mkandarasi huyu anaanza kujenga hiyo barabara ya Karatu – Haydom – Maswa? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, pamoja na barabara nyingi ambazo ziko takribani sita, ziko kwenye EPC+F, baada ya kusaini nilijibu hapa kwamba, wakandarasi wameendelea kuoneshwa hayo maeneo na barabara hizi zinasimamiwa na makao makuu.

Mheshimiwa Spika, kinachofanyika sasa ikiwepo na hiyo barabara ambayo inapita kwenye Jimbo la Mheshimiwa Mbunge, ni kuwaonesha wakandarasi, wakandarasi kuzigawa zile barabara kwenye vipande (lots) zaidi ya nne na kutafuta wakandarasi wengine ambao watasimamiwa na huyo mkandarasi mkubwa kwa ajili ya kujenga hizo barabara. Kutakuwa na vipande visivyopungua vinne katika kila barabara, kwa maana ya makambi, kutafuta maeneo ambayo yana raw materials, kwa maana ya kokoto na changarawe, tayari wako wanapita na kujitambulisha kwenye hizo barabara. Kwa hiyo, mchakato unaendelea, ahsante.

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Njia Panda - Mangola - Matala hadi Lalago kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona; barabara ya Pachayamindu – Ngapa kuelekea Nachingwea, ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama, je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge, Serikali inatafuta fedha ili kwanza iweze kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, baada ya hapo gharama itajulikana na Serikali itafuta fedha kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Njia Panda - Mangola - Matala hadi Lalago kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, je, ni lini kipande cha barabara cha kuanzia Malagarasi – Mpeta mpaka Uvinza kitakamilishwa kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ni kusimamia utekelezaji, kwa sababu hicho kipande alichokitaja cha kilometa 51.3, Mkandarasi yuko site, tukisaidiana na mwenzetu wa Abu Dhabi. Kwa hiyo, ni suala tu la kuwasimamia kuhakikisha kwamba wanakwenda kwa kasi ili kiweze kukamilika, maana ndiyo kipande pekee kilichobaki cha vumbi kutoka hapa hadi Kigoma. (Makofi)

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Njia Panda - Mangola - Matala hadi Lalago kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 9

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mpanda – Uvinza – Kasulu? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ahsante, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge, barabara hii tumeshakamilisha usanifu na itakuwa ndiyo barabara kuu ya kutoka Kusini kwa maana ya Mpanda – Uvinza hadi Kasulu ambayo haizidi kilometa 57.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kweli inatafuta fedha ili iweze kukamilisha hicho kipande ambacho ndiyo kimebaki peke yake katika Mkoa wa Kigoma, barabara kuu ambayo haina lami. Kwa hiyo, tunalifahamu na Serikali imeendelea kutafuta fedha ili kukamilisha kipande hicho kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Njia Panda - Mangola - Matala hadi Lalago kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 10

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, ninaomba kujua Mheshimiwa Naibu Waziri umepita sana barabara ya Sanzati kwenda Nata. Sasa ni lini hiyo barabara itamalizika maana imekuwa kero kwa wananchi wa Bunda? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba nichukue nafasi hii kusema kwamba, Mkandarasi tayari yuko site anafanya kazi. Nawahimiza Watendaji wa TANROADS pamoja na Meneja wa Mkoa ambao wanamsimamia Mkandarasi, kuhakikisha kwamba wanamsimamia ili aongeze kasi na kukamilisha barabara hiyo ambayo inahitajika sana kwa wananchi wa Bunda pia wananchi wa Wilaya ya Serengeti.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Njia Panda - Mangola - Matala hadi Lalago kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 11

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, nashukuru, miradi ambayo itaendeshwa na the so-called EPC+F, ni programu ambayo ililetwa na Serikali hapa Bungeni, lakini majibu ya Waziri unavyojibu ni kama vile huna uhakika hizi barabara zitakamilika lini. Sasa unataka kutuambia wakati mnaandaa hiyo programu, mlikuwa hamjajua zile barabara mlizolenga changamoto zake zikoje, mahitaji yake yakoje na yatafanikiwa vipi? Maana majibu yako hayaeleweki.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imekuja na mpango huu uko kwenye bajeti na inajua itafanyaje, lakini mpango mpya kabisa katika nchi yetu. Kwa hiyo, kinachofanyika na ndiyo taratibu zake kwamba unakuwa na Mkandarasi mmoja katika kila barabara, mkandarasi mkubwa kwa sababu barabara ni ndefu, anakuwa na sub-contractors ambao ni lazima ajiridhishe na afanye tathmini pia ya kwake kwa sababu, yeye ndiye anayesimamia ujenzi wa zile barabara, kwa maana yote kwamba EPC (Engineering Procurement) na yeye ndiyo anayefanya pia procurement. Kwa hiyo, lazima baada ya kumkabidhi ile barabara ajiridhishe namna pia atakavyogawa hizo barabara.

Mheshimiwa Spika, kazi ya Serikali ni kumpa fedha na kazi hizo zinaendelea, walioko kwenye zile barabara sasa hivi wako wanaoneshwa zile barabara. Kwa hiyo, watakapoanza, watakuwa pia wamejiridhisha maana yake baada ya kukubaliana hakutakuwa na variation kwenye hizo barabara, ahsante. (Makofi)