Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 9 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 131 2023-09-08

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Njia Panda - Mangola - Matala hadi Lalago kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Tlemai Awack, Mbunge wa Karatu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Njia Panda kuanzia Karatu – Mang’ola – Matala – Sibiti River hadi Lalago, yenye urefu wa kilometa 328 inayojulikana kama Eyasi Route.

Mheshimiwa Spika, sehemu ya kuanzia Sibiti River hadi Lalago yenye urefu wa kilometa 121 imejumuishwa kwenye mradi wa EPC+F kupitia barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti River – Lalago hadi Maswa ambayo ina jumla ya kilomita 389 ambapo mkataba wake wa ujenzi umesainiwa. Kwa sehemu iliyobaki ya Njia Panda – Mang’ola hadi Matala kilometa 137, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi, ahsante (Makofi)