Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini huduma ya Mawasiliano ya Simu itapelekwa Kata za Bwawani, Oldonyowas, Laroi, Mwandet, Oljoro na Oldonyosambu?

Supplementary Question 1

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, Kata ya Kirogo wananchi wa Kata hii ili kufanya mawasiliano wakati mwingine huwalazimu kupanda juu ya milima, na kwa kuwa Kata hii ipo kwenye ile miradi ya kidigitali, ninataka nijue commitment ya Serikali, ni lini miradi hii itaanza ya ujenzi wa minara kwenye Kata hii ya Kirogo? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, mradi huu umeshaanza na upo katika hatua mbalimbali. Tunaamini kwamba Jimbo la Rorya watafika kwa ajili ya utekelezaji huo, ahsante sana. (Makofi)

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini huduma ya Mawasiliano ya Simu itapelekwa Kata za Bwawani, Oldonyowas, Laroi, Mwandet, Oljoro na Oldonyosambu?

Supplementary Question 2

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Kiteto ilikuwa na vijiji vingi sana, sasa kwa mujibu wa mikataba indication ni lini, walikubaliana watamaliza kwa kipindi gani? Kwa sababu kesho nina mkutano wa hadhara na haya maswali yatakuwa mengi sana.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Advocate Olelekaita, Mbunge wa Kiteto kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu kwenye baadhi ya maswali ni kwamba utekelezaji wa miradi hii ya minara 758 kuna hatua kadhaa ambazo zinafanyika na mkataba wetu ukamilishaji wake utaanzia kwenye miezi tisa. Kuna maeneo ndani ya miezi tisa minara itakuwa imeshakamilika na kuna maeneo katika miezi 10, 11 mpaka mwisho wa mkataba wetu itakuwa ni miezi 20 tutakuwa tumehakikisha kwamba minara imeshasimama katika maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, kikubwa sana ili kuhakikisha kwamba Serikali inaendelea ku-monitor utekelezaji, tumehakikisha kwamba tumewapatia utaratibu maalum, kila baada ya miezi mitatu wanatoa taarifa ya utekelezaji walipofikia na mpaka sasa watoa huduma wengi wameshatupatia utekelezaji wao, wengine wameshapata vibali, wengine wameshapata benki guarantee, kuna wengine bado hawajapata benki guarantee.

Kwa hiyo, watoa huduma mbalimbali wako katika hatua mbalimbali, lakini wako ndani ya muda ambao tumekubaliana. Nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge pamoja na Watanzania kwamba utekelezaji huu utaenda kama ambavyo umepangwa.

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini huduma ya Mawasiliano ya Simu itapelekwa Kata za Bwawani, Oldonyowas, Laroi, Mwandet, Oljoro na Oldonyosambu?

Supplementary Question 3

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, je, ni lini Serikali itapeleka minara katika Kijiji cha Misyaje, Kata ya Malumba?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kwanza kabisa nipokee changamoto hii ya mawasiliano kutoka kwenye hiyo kata, lakini nimwombe Mheshimiwa Mbunge kwa sababu sina taarifa za kina kuhusu kata hiyo ili tuweze kuitazama na kwenda kuchukua hatua stahiki, nakushukuru sana.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini huduma ya Mawasiliano ya Simu itapelekwa Kata za Bwawani, Oldonyowas, Laroi, Mwandet, Oljoro na Oldonyosambu?

Supplementary Question 4

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya mawasiliano katika Kata ya Sirop, Wilaya ya Hanang?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia Halamga, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Manyara kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa Kata ya Sirop ina changamoto ya mawasiliano. Nimwombe tu Mheshimiwa Mbunge baada ya kikao hiki cha Bunge tukutane ili nimuunganishe na watalam wetu ili waweze kumpa tarehe ya kufika katika eneo hilo kwa ajili ya kufanya tathmini, nakushukuru sana.

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini huduma ya Mawasiliano ya Simu itapelekwa Kata za Bwawani, Oldonyowas, Laroi, Mwandet, Oljoro na Oldonyosambu?

Supplementary Question 5

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, swalil a kwanza; kwa kuwa wananchi katika karne hii ya leo wanateseka kupanda juu ya vichuguu na vilima kutafuta mawasiliano; je, tathimini hii itafanyika ili wananchi hawa wapate huduma? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kwa kuwa Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan aliwapa Wizara hii minara mia saba na hamsini na nane.

Je, sasa Wizara haioni ni wakati muafaka Kata za Oldonyowas, Oldonyosambu, Mwandet, Laroi, Oljoro na Bwawani kupata mgao wa minara hiyo? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Noah, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba Watanzania hawapandi kwenye miti, hawapandi kwenye vichuguu ili kupata huduma ya mawasiliano na ndiyo maana Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan inajitahidi sana kutafuta fedha ili kuhakikisha kwamba inatatua changamoto hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kipengele cha pili cha swali la Mheshimiwa Mbunge, ili kufikia kwenye miradi kutangazwa na zabuni kupatikana hatua ya kwanza tunaanza na kufanya tathmini ili kujiridhisha tatizo likoje, tunafanya feasibility study, baada ya hapo tunafanya detailed design na baada ya hapo tunakuja kutangaza tender, sasa hatua ambayo imefikiwa ambayo Mheshimiwa Mbunge ameiongelea ni hatua ya kusaini Mkataba ambapo tayari pesa zimeshaelekezwa katika maeneo maalum.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge jambo moja kwamba, Serikali tayari imeshapata fedha kwa ajili ya kufanya tathmini katika maeneo yake na tukishakamilisha na fedha zikapatikana, basi tutatangaza tender kwa ajili ya kufikisha huduma ya mawasilino kwa ajili ya wananchi wa Arumeru Magharibi, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Aloyce Andrew Kwezi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini huduma ya Mawasiliano ya Simu itapelekwa Kata za Bwawani, Oldonyowas, Laroi, Mwandet, Oljoro na Oldonyosambu?

Supplementary Question 6

MHE. ALOYCE A. KWEZI: Mheshimiwa Spika, napenda kuuliza swali; katika Jimbo la Kaliua kuna Kata ambazo ziko kwenye programu ya kupata mawasiliano ya simu hususani Iyagala, Isawima pamoja na Ugunga; je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kuweka minara katika eneo hilo? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Kaliua, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa ujenzi wa minara katika maeneo mbalimbali nchini unaendelea na uko katika hatua mbalimbali. Nimhakikishie kabisa Mheshimiwa Mbunge kwamba, tumetoa maelekezo kwa watoa huduma, ndani ya Mkataba ambao tumekubaliana nao, hatutowaacha ifike miezi ishirini ndiyo tuseme kwamba umekamilisha au haujakamilisha. Tumepeana kwamba kila baada ya muda fulani watupatie taarifa ya utekelezaji wamefikia wapi ili tuweze ku-monitor na ku-evaluate kadri mradi wa utekelezaji unavyoenda. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuhusu Jimbo la Kaliua utekelezaji utaendelea na sisi Serikali tunalitazama kwa makini sana ili wananchi wa Kaliua waendelee kupata huduma ya mawasiliano, nakushukuru sana.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini huduma ya Mawasiliano ya Simu itapelekwa Kata za Bwawani, Oldonyowas, Laroi, Mwandet, Oljoro na Oldonyosambu?

Supplementary Question 7

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Changamoto za mawasiliano zilizopo Arumeru Magharibi zinafanana sana na hali ilivyo kule kwetu Mashariki.

Je, ni lini Serikali itaondoa kabisa changamoto za mawasiliano katika Kata za pembezoni Ngarenanyuki, Leguruki, Maruvango, King’ori na Malula? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa sababu Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan inawapenda Watanzania na kwa sababu inataka Watanzania wote washiriki katika uchumi wao wa kidigitali na ni lazima wawasiliane kwa kutumia mifumo ya TEHAMA na sisi kama Serikali ambao ni wasaidizi wa Mheshimiwa Rais, najitolea kuhakikisha kwamba nitaenda katika Jimbo la Arumeru Mashariki ili tukajionee changamoto ilivyo na tuchukue hatua na hakuna cha kwamba ni kata moja tu, tutahakikisha maeneo yote ambayo yana changamoto kulingana na upatikanaji wa fedha tutafikisha mawasiliano, ahsante sana. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini huduma ya Mawasiliano ya Simu itapelekwa Kata za Bwawani, Oldonyowas, Laroi, Mwandet, Oljoro na Oldonyosambu?

Supplementary Question 8

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, Je, ni lini Serikali itajenga minara ya simu Kata ya Mapanda na Kibengu katika Jimbo la Mufindi - Kaskazini kwa sababu wananchi wanapata shida sana ya mawasiliano? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, maeneo ya Kibengu hayapo katika minara 758 lakini tunayaingiza kwenye tathmini ya minara kwenye vijiji 2,116. Kwa hiyo, tukishakamilisha na fedha zikapatikana, tutafikisha mawasiliano katika Kata hiyo, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini huduma ya Mawasiliano ya Simu itapelekwa Kata za Bwawani, Oldonyowas, Laroi, Mwandet, Oljoro na Oldonyosambu?

Supplementary Question 9

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, Kata ya Ilolanguru, Kata ya Ikobe, Kata ya Iponya na Lubembela zinakabiliwa na changamoto ya mawasiliano. Waziri lini utapeleka mawasiliano Wilaya ya Mbogwe katika Kata hizo nilizozitaja? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, maeneo yaliyotajwa na Mheshimiwa Maganga kuna maeneo ambayo yanafanyiwa tathmini lakini kuna maeneo ambayo yapo ndani ya miradi 758. Kwa hiyo, nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge miradi hii itakapokamilika lakini na yale ambayo tumeyaingiza kwenye tathmini na fedha zikapatikana tutafikisha mawasiliano ndani ya Jimbo la Mbogwe. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini huduma ya Mawasiliano ya Simu itapelekwa Kata za Bwawani, Oldonyowas, Laroi, Mwandet, Oljoro na Oldonyosambu?

Supplementary Question 10

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; je, ni lini Serikali itajenga minara ya simu Jimbo la Ngara, Kata ya Murukulazo kwa sababu mawasiliano yanasuasua? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa eneo hilo lina changamoto kwa sababu liko mpakani kule na linapata huduma kutoka maeneo ya ndani ambapo minara yake haina nguvu sana. Tulishatuma wataalam wetu katika maeneo haya kwa sababu yapo katika miji ambayo ni ya kimkakati na Serikali imejipanga kuhakikisha kwamba, maeneo yote ya kimkakati tunahakikisha tunaimarisha huduma ya mawasiliano. Kwa hiyo, nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge tunalifanyia kazi. (Makofi)

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini huduma ya Mawasiliano ya Simu itapelekwa Kata za Bwawani, Oldonyowas, Laroi, Mwandet, Oljoro na Oldonyosambu?

Supplementary Question 11

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itaanza kujenga minara 15 iliyopangwa kujengwa katika Wilaya ya Kilwa? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, tayari mradi wa Tanzania ya kidigitali minara 755 kwenda kwenye kata 713, Wilaya 112. Ninakuhakikishia kwamba iko katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Hivyo ninamuomba Mheshimiwa Mbunge tuwe na subira kwa sababu ujenzi wa minara ni hatua, hatua hizo zikishakamilika kusimamisha mnara wenyewe hauchukui hata miezi miwili. Kwa hiyo, ninamuomba Mheshimiwa Mbunge tuendelee kutoa ushirikiano katika maeneo ambapo wataalamu wetu watakapofika kwa ajili ya kupata maeneo na vibali basi awe sehemu ya ufanikishaji huo. Nakushukuru sana. (Makofi)