Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Spika, majibu ya Serikali kidogo yana changamoto kwa wastaafu hawa wa Afrika Mashariki, kwa sababu wastaafu hawa wamefungua kesi na ni imani yangu kwamba Serikali inafahamu kesi ya wastaafu hawa.

Je, Serikali iko tayari kuwaeleza wastaafu hawa kwamba malipo yao yalishalipwa na waache kushughulikia kesi yao?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; wazee hawa wamekuwa wakihangaika kwa muda mrefu kufuatilia malipo haya lakini Serikali inasema imewalipa mpaka mwaka 2016 madeni haya yameshalipwa. Sasa Serikali hawa wazee wanadai kitu gani mpaka wamekuwa wakihangaika mpaka kufungua kesi mbalimbali katika mahakama tofauti ili wapate stahiki zao?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, ni kweli kama alivyosema wastaafu hawa ambao kwa kweli kimsingi kama nilivyosema kwenye jibu la msingi walishalipwa na imekuwa ni tendency au kawaida kila kunapokuwa na Serikali mpya au regime mpya wanafungua madai katika mahakama yetu kudai malipo, lakini kimsingi Serikali tumeshasema na tunaelekeza tena kwamba kwa kweli waelewe kwamba walishalipwa na hakuna kingine zaidi kwa sababu tayari tulishamaliza kama nilivyosema. Kwa hiyo, wasiendelee tena na madai ambayo kimsingi hayana ukweli.

Mheshimiwa Spika, wastaafu hawa hawadai chochote kama nilivyosema walishalipwa kila kitu na tunachoendelea kulipa sasa ni pensheni kwa wale wachache ambao wanastahili kulipwa pensheni, nakushukuru. (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi ni kuweka tu msisitizo kwamba wananchi wetu wana haki ya kwenda mahakamani wanapoona wanaweza wakapata haki zaidi, lakini kwa maana ya Serikali ilishahitimisha mchakato huu kwa barua na waliandikiwa barua ya tarehe 31 Desemba, 2013 ya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha wanayo, lakini hiyo haizuii wananchi kuwa na haki ya kwenda mahakamani. Kwa hiyo, Serikali haiwezi kuzuia wananchi kwenda mahakamani, lakini kwa maana ya mchakato ulishafanyika, ukahitimishwa kwa barua na iliandikwa, ahsante.

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki?

Supplementary Question 2

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, ahsante; je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia na kuharakisha malipo ya waliokuwa wafanyakazi wa mashamba ya maua ya P Floral ili kupisha mwekezaji mpya? Ahsante sana.

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, nitamwona Mheshimiwa Zaytun Swai pia kama itakuwa kuna ulazima basi alete swali la msingi.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, kwa nini Serikali isiweke mfumo kwa wastaafu na ukajulikana kabisa kulikoni kusumbuliwa kuleta barua kila wakati wanapodai madai yao?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali tayari imekwishakuweka utaratibu kupitia mifuko ya pensheni. Sasa hivi hakuna hitaji la kwamba apeleke taarifa zake, tayari tumeshaweka utaratibu ambao moja kwa moja mtumishi anapoelekea kwenye kustaafu miezi sita kabla taarifa zake zinaanza kuandaliwa na sasa tunatoa pensheni yake ndani ya siku 60 na kama hakuna dosari yoyote hata siku tatu anapata mafao yake. Kwa hiyo, changamoto hiyo tumekwishaitatua.