Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 9 Planning and Investment Ofisi ya Rais: Mipango na Uwekezaji 125 2023-09-08

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki?

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, madai ya wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliidhinishwa na kulipwa kupitia Waraka wa Baraza la Mawaziri Na. 39 wa mwaka 2006. Serikali iliamua kuwalipa wastaafu hao kwa kuzingatia Sheria za Pensheni za Jumuiya hiyo, sheria na taratibu za fedha, maridhiano ya mwaka 1984 na Sheria Na. 2 ya mwaka 1987, pamoja na Hati ya Makubaliano ya Septemba, 2005 na Hukumu ya Mahakama Kuu ya tarehe 21 Septemba, 2005.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia miongozo tajwa hapo juu Serikali iliandaa utaratibu wa kuwalipa wastaafu na mirathi kwa waliofariki wapatao 31,831 kwa mujibu wa Hati za Makubaliano. Zoezi hilo lilifanyika kwa kipindi cha miaka minane kuanzia Julai, 2006 hadi Novemba, 2013 lilipofungwa rasmi.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali inaendelea kulipa pensheni za kila mwezi kwa wastaafu ambao hawakuwa kwenye mpango wa kuchangia ambao walirejeshwa na kusajiliwa katika daftari la malipo ya pensheni ya kila mwezi. Kwa mwaka wa fedha 2023/2024 hadi kufikia Septemba, 2023 Serikali imeshalipa shilingi 1,075,289,494.12 kwa wastaafu 1,744.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kulipa pensheni kwa wastaafu wanaostahili kulingana na sheria, kanuni na taratibu za malipo ya Serikali na si vinginevyo, nakushuru.