Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa jengo la Mahakama Wilayani Mbulu?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa Mahakama ya Mwanzo ya Usanda katika Wilaya ya Shinyanga imechakaa. Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Mahakama hiyo?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Mnzava, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika Mkoa wetu wa Shinyanga tunakwenda kujenga katika mwaka huu wa fedha katika Tarafa ya Majengo, Kata ya Malunga naomba ni-check na Mheshimiwa Dkt. Mnzava ili tuone kwamba Mahakama hiyo ambayo imechakaa tuweze kuingiza kwenye mpango unaofuata wa Mahakama ya ujenzi. Ahsante.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa jengo la Mahakama Wilayani Mbulu?

Supplementary Question 2

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kuniruhusu niulize swali la nyongeza. Wilaya ya Uyui ni mpya na hatuna Mahakama, tunatumia chumba kidogo sana; je, lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya ya Uyui?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru na naomba nijibu swali la Mheshimiwa Maige, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mpango wetu wa kujenga Mahakama za Wilaya ni pamoja na kukarabati ambazo ni chakavu, naomba nipokee Mahakama hii ya Uyui nita-check na Mheshimiwa Mbunge tuone tuiweke kwenye mpango ili tuweze kukarabati pia.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa jengo la Mahakama Wilayani Mbulu?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Tarafa ya Heru Juu iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Kasulu haina Mahakama, inafanyia kazi katika Ofisi ya Mtendaji. Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama katika Tarafa ya Heru Juu? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru na naomba sasa nijibu swali la Mheshimiwa Genzabuke, Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, naomba nimjulishe Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mpango wetu wa kujenga Mahakama 60 kote nchini katika bajeti ya mwaka huu, ambayo mlitupitishia, Tarafa ya Heru Juu, Kata ya Heru Juu iko katika list hiyo Mheshimiwa Mbunge tunakwenda kujenga mwaka huu wa fedha. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa jengo la Mahakama Wilayani Mbulu?

Supplementary Question 4

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa muda mrefu imekuwa na mpango wa kujenga Mahakama ya Mwanzo Kata ya Izigo, Wilaya ya Muleba, ningependa kujua utekelezaji wa ujenzi wa Mahakama hiyo umefikia wapi? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru na naomba nijibu swali la Mheshimiwa Oliver Semuguruka, Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika Mkoa wetu wa Kagera katika Wilaya ya Muleba Kata hii ya Izigo, Tarafa ya Izigo iko kwenye mpango wa mwaka huu, tunakwenda kujenga mwaka huu Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa jengo la Mahakama Wilayani Mbulu?

Supplementary Question 5

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, Mahakama ya Mwanzo ya Machame ilisimamishwa kwa kipindi kirefu kutokana na uchakavu wa majengo, lakini kwa kushirikiana na wadau tumejenga, tumefanya ukarabati wa Mahakama hiyo ya Mwanzo ya Machame na imekamilika na jengo liko pale.

Je, ni lini sasa mtapeleka Hakimu pale ili aweze kuanza kutoa huduma?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru na naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Saashisha, amechangia katika Mfuko wake wa Jimbo kuhakikisha lile jengo la Mahakama pale Hai – Machame linakarabatiwa, lakini tatizo tulilonalo pale lile jengo bado lina crack nyingi, Mheshimiwa anafahamu hilo.

Mheshimiwa Spika, katika mpango wetu wa Mahakama tumetenga fedha kwenye Kata hiyo ya Machame tunakwenda kujenga eneo lingine. Ninamuhaidi Mheshimiwa Mbunge tutakwenda pale Hai – Machame tuone hilo eneo ambalo lina-disputes hilo ambalo jengo limechakaa na pale ambako tunataka kujenga tutafikia consensus wapi tujenge, ahsante.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa jengo la Mahakama Wilayani Mbulu?

Supplementary Question 6

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali na hatua hiyo ya kuanza ujenzi. Mimi nina swali moja tu.

Mheshimiwa Spika, katika Tarafa ya Nambisi kuna Mahakama chakavu katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu. Je, utaratibu wa Serikali ukoje wa kukarabati majengo ya Mahakama katika Tarafa zetu nchini?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru na nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa pongezi hizo.

Mheshimiwa Spika, mhimili wetu wa Mahakama una mpango wa miaka mitano wa kukarabati na kujenga majengo ya Mahakama kote nchini na katika mpango huu Mtendaji Mkuu wa Mahakama akishirikiana na Watendaji wa Mikoa wanafanya wanafanya utafiti katika Tarafa zote nchini zaidi ya Tarafa 500 na Kata zaidi ya 3,000 kuona ni wapi ambapo kuna mashauri mengi na umbali, tafiti hii tutakapokamilisha tutakuja sasa na list ya kwamba wapi tuanze.

Mheshimiwa Spika, ninafahamu kwamba hata Nambisi ambako Mheshimiwa Mbunge amepataja kuna uhitaji naomba avute subira tuweze kukamilisha tafiti hii halafu tutamwambia kama hapo tutakwenda kujenga. (Makofi)