Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 8 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 120 2023-09-07

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa jengo la Mahakama Wilayani Mbulu?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ninakushukuru na pia ninamshukuru Mwenyezi Mungu, na naomba sasa kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria niweze kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mahakama ya Wilaya ya Mbulu kwa sasa inaendeshwa katika jengo ambalo ni chakavu na finyu sana kukidhi mahitaji. Aidha, jengo hilo pia lipo kwenye eneo la hifadhi ya barabara na hivyo linapaswa kuondolewa. Katika mpango wetu wa ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Mbulu itajengwa katika mwaka wa fedha 2023/2024 na tayari mshauri elekezi ameshakamilisha usanifu na maandalizi ya zabuni kwa ajili ya kupata mkandarasi wa ujenzi. Ujenzi unatarajia kuanzia mwezi Septemba, 2023 na kukamilika kabla ya Juni, 2024.