Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kassim Hassan Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanakwerekwe

Primary Question

MHE. KASSIM HASSAN HAJI aliuliza: - Je, lini Serikali itafanya maboresho ya Sheria ya Mfuko wa Jimbo ili kuondoa kikwazo cha utekelezaji Zanzibar kwa kuwa Wabunge siyo Madiwani?

Supplementary Question 1

MHE. KASSIM HASSAN HAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa kodi inayokatwa katika matumizi ya mfuko huu ni kubwa sana, ni lini Serikali itaenda kuondoa kodi hiyo katika matumizi ya Mfuko wa Jimbo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa Wakurugenzi wetu wengi ni wapya ambao wamechaguliwa katika kuendesha halmashauri zetu. Je, ni lini Serikali itakwenda kupeleka mafunzo kuwawezesha Wakurugenzi hawa kujua thamani ya Mfuko wa Jimbo kwa Waheshimiwa Wabunge? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kassim Hassan Haji, Mbunge wa Mwanakwerekwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza, naomba tulipokee suala la kodi inayokatwa katika fedha za Mfuko wa Jimbo na hususan kwa upande wa Zanzibar. Suala hili ni la kiutaratibu, tutafanya utaratibu kuhusiana na Wizara ya Fedha lakini pia Wizara ya Muungano, Ofisi ya Rais TAMISEMI, kwa pamoja tuweze kuona njia nzuri zaidi ya kurekebisha changamoto hii ili tuweze kwenda vizuri zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la pili kuhusiana na Wakurugenzi wengi kuwa wapya. Ni kweli na tunahitaji kuona Wakurugenzi wetu wanaelewa vizuri wajibu wao wa kutekeleza Mfuko wa Jimbo. Nitumie fursa hii kwanza, kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tutafanya mafunzo kwa Wakurugenzi wote ili wajue wajibu wao katika kusimamia Mfuko wa Jimbo.

Mheshimiwa Spika, natoa msisitizo kwa Wakurugenzi wote kote nchini, kumekuwa na changamoto, Waheshimiwa Wabunge wanakaa na Kamati za Mfuko wa Jimbo, wanapitisha miradi lakini Wakurugenzi wanazuia fedha zisiende kutekeleza miradi ile.

Mheshimiwa Spika, naomba kutumia fursa hii kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, kuelekeza kwamba Mkurugenzi yeyote atakayekiuka utaratibu baada ya Mwenyekiti wa mfuko huo kuidhinisha matumizi, tutachukua hatua kali za kinidhamu dhidi yake. Miradi hii itekelezwe kwa wakati baada ya Waheshimiwa Wabunge kupitisha miradi hiyo. Ahsante. (Makofi)

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. KASSIM HASSAN HAJI aliuliza: - Je, lini Serikali itafanya maboresho ya Sheria ya Mfuko wa Jimbo ili kuondoa kikwazo cha utekelezaji Zanzibar kwa kuwa Wabunge siyo Madiwani?

Supplementary Question 2

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa fedha za Mfuko wa Jimbo zinategemea sana idadi ya watu kwenye majimbo yetu, na ni ukweli sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 imekamilika na hivyo tunazo takwimu mpya kwenye majimbo yetu.

Je, katika mwaka wa fedha 2023/2024 fedha zitakazotolewa zitazingatia idadi ya watu kwenye majimbo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba fedha za Mfuko wa Jimbo zinategemea idadi ya wananchi katika jimbo husika, ukubwa wa kijiografia lakini pia na kasi ya umaskini katika eneo husika.

Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kwanza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kipindi cha mwaka wa fedha uliopita iliongeza fedha za Mfuko wa Jimbo. Waheshimiwa Wabunge wote ni mashahidi; iliongezeka na imeendelea kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa miradi hiyo. Suala la kuzingatia matokeo ya sensa ya mwaka jana ni muhimu na Serikali itaendelea kufanya kazi kwa sababu moja ya kigezo ni idadi ya watu katika maeneo hayo. (Makofi)