Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 114 2023-09-07

Name

Kassim Hassan Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanakwerekwe

Primary Question

MHE. KASSIM HASSAN HAJI aliuliza: -

Je, lini Serikali itafanya maboresho ya Sheria ya Mfuko wa Jimbo ili kuondoa kikwazo cha utekelezaji Zanzibar kwa kuwa Wabunge siyo Madiwani?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Haji Kassim, Mbunge wa Mwanakwerekwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Mfuko wa Jimbo Na. 16 ya mwaka 2009, uidhinishwaji wa vipaumbele na matumizi ya fedha hufanywa na Kamati ya Mfuko wa Jimbo yenye wajumbe saba, akiwemo Mbunge wa Jimbo husika ambaye ndiye Mwenyekiti wa Kamati. Aidha, Kamati ina jukumu la kupokea, kujadili vipaumbele vya miradi iliyowasilishwa na wananchi na kuidhinisha miradi itakayotekelezwa.

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Mfuko wa Kuchochea Maendeleo ya jimbo inatekelezwa sambamba na Sheria ya Fedha, Sheria ya Manunuzi ya Umma pamoja na Miongozo mbalimbali ya Mipango, Bajeti na Matumizi ya fedha za Umma. Hivyo, utaratibu uliopo kisheria unamwezesha Mbunge wa Jimbo husika kutimiza wajibu wake wa kupokea maombi, kuweka vipaumbele na kuidhinisha fedha kwa ajili ya utekelezaji wa vipaumbele vilivyokubaliwa, ahsante.