Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza kutekeleza mradi wa maji wa Ziwa Victoria kwenda vijiji na vitongoji vya Kata za Nguvumoja, Lugubu na Itumba – Igunga?

Supplementary Question 1

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Wakati wa usanifu wa maji kutoka Igunga kwenda Shelui wataalam wa Wizara waliwaaminisha wananchi kwamba yangetengenezwa matoleo kwa ajili ya kusambaza maji kwenye hizi kata ya Nguvumoja, Lugubu na Itumba lakini mradi umekamilika na matoleo ya maji hayajawekwa na wananchi hawajapata maji.

Je, Wizara hamuoni kutokutekeleza kwa kipengele hichi ni kuwachonganisha wananchi na Serikali yao sikivu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa kuwa Wizara mmekuwa na utaratibu wa kutoa fedha kwa matokeo (P4R) na Mkoa wa Tabora tunafanya vizuri sana.

Je, hamuoni ni wakati sasa mtoe fedha ili kwenda kukamilisha huu mradi ili wananchi waendelee kuwa wanafurahia Serikali yao ya Chama cha Mapinduzi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Awali ya yote ninapenda kukupongeza Mheshimiwa Ngassa kwa ufuatiliaji, lakini Mheshimiwa Ngassa Wizara hata siku moja haitaweza kuwa chonganishi kati ya Serikali na wananchi, tutaweza kufanya kwa bidii kubwa sana kuhakikisha Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mama mwenye uchungu wa wanawake wanaobeba ndoo kichwani inatekeleza miradi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutotoa matoleo ni sababu za kiufundi Mheshimiwa Mbunge, wakati fulani wakati usanifu unafanyika tulitarajia ingewezekana lakini population ya watu Tanzania sasa hivi inakua kila leo, kwa hiyo usanifu huu mpya utaleta maji ya kutosha na yatakuwa endelevu kwa eneo zima hili la Igunga.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu P4R tuna kila sababu ya kumshukuru na kumpongeza sana Dkt. Samia, tulikuwa na Mikoa 17 pekee yenye kupata fedha za P4R lakini sasa hivi ni Mikoa yote 25 Mheshimiwa Rais Dkt. Samia amepambana fedha zimepatikana kwa Mikoa yote, na eneo la Tabora kama ulivyosema linafanya vizuri tayari fedha pia zimeanza kupelekwa na fedha zimeongezeka. Kwa hiyo, ninakutoa hofu, hili mimi na wewe naomba tuonane ili tuweze kuweka sawa. (Makofi)

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza kutekeleza mradi wa maji wa Ziwa Victoria kwenda vijiji na vitongoji vya Kata za Nguvumoja, Lugubu na Itumba – Igunga?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mradi wa maji wa Usalimwani - Mvumbi, Kitulo- Ijuni, Kidepwe - Madihani, Mariwa - Ikete ni miradi ambayo imesimama. Ni lini Serikali itatoa fedha ili miradi hii iweze kukamilika kwa ajili ya wananchi wa Wilaya ya Makete?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sanga, Mbunge machachari kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, fedha tayari zimeanza kutoka wiki hii, tutarajie hata Wakandarasi wanaofanya miradi hiyo aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge watalipwa.