Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 85 2023-09-05

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza kutekeleza mradi wa maji wa Ziwa Victoria kwenda vijiji na vitongoji vya Kata za Nguvumoja, Lugubu na Itumba – Igunga?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nicholaus George Ngassa, Mbunge wa Igunga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu spika, katika jitihada za kuboresha huduma ya maji safi na salama kwenye Kata za Nguvumoja, Lugubu na Itumba zilizopo Wilaya ya Igunga, Serikali inatekeleza mipango ya muda mfupi na muda mrefu, ambapo katika mpango wa muda mfupi kwa mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali itafunga pampu za kutumia Nishati ya umeme jua katika visima virefu vya Vijiji vya Nguvumoja, Mwanshoma, Lugubu na Itumba ili kuimarisha upatikanaji wa huduma ya maji na kupunguza gharama za uendeshaji wa miradi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia, Serikali imepanga kufanya utafiti wa maji ardhini na kuchimba kisima kirefu katika Kijiji cha Chagana kilichopo Kata ya Lubugu katika kipindi cha Mwezi Desemba, 2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mpango wa muda mrefu, Serikali itaboresha huduma ya maji safi na salama na yenye kutosheleza katika Kata za Nguvumoja, Lugubu na Itumba – Igunga kwa kutumia mradi wa maji wa Ziwa Victoria ambapo upembuzi yakinifu na usanifu wake wa kina umekamilika na utaanza utekelezaji mara fedha zitakapopatikana.