Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya mchepuo kwenda Moshi kupitia Chekereni – Kahe – Mabogini - TPC kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHARLES. S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kwamba Serikali imetoa majibu mazuri na nimeyafurahia sana, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, Bodi ya Barabara ya Mkoa wetu wa Kilimanjaro imeshatuma maombi kwenye Wizara ya kuipandisha hadhi Barabara hii ya Chekereni – Kahe – Mabogini – TPC.

Je, tutapata uthibitisho gani kwamba maombi haya yameshughulikiwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, nashukuru sana Serikali imeweza kutengeneza Daraja la Marangu Mtoni; lakini tunaomba kauli ya Serikali kuhusiana na kukamilisha kipande kilichobaki cha barabara hiyo kuanzia Kawawa – Nduoni kuja Marangu Mtoni ambayo ipo pia kwenye Ilani ya CCM, ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Charles Stephen Kimei, Mbunge wa Vunjo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza ni juu ya Bodi ya Barabara kuipandisha hadhi Barabara ya Kahe – Chekereni. Suala hili ni la kisheria na taratibu za namna ambavyo barabara inatakiwa kupandishwa hadhi na kwenda kwa wenzetu wa Wizara ya Ujenzi zipo wazi. Hivyo basi, tutakaa na Mheshimiwa Kimei kuona ni hatua zipi ambazo maombi haya yamefikia ili kuona kama tayari yamefika kwa Waziri wa Ujenzi mwenye dhamana ya kupandisha hadhi barabara hii. Kama maombi haya hayajafika basi tutaona ni namna gani yanaweza kufika ili timu iweze kwenda kufanya assessment na barabara hii iweze kupandishwa hadhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naenda kwenye swali lake la pili linalohuau Saraja la Marangu Mtoni, ambalo linaunganisha barabara ya Kawawa – Kahe – chekereni. Nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa Vunjo, kwamba Serikali ya Awamu ya Sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mwaka wa fedha 2023/2024 imetenga zaidi ya shilingi milioni 989 kuhakikisha kwamba barabara katika jimbo la Mheshimiwa Kimei zinafanyiwa ukarabati ikiwemo Barabara hii ambayo inaitwa Fungate – Mabogini – Kahe – Chekereni ambapo kwa sasa kuna shilingi milioni 39. Inasubiri tu daraja lile likamailike ili barabara nayo iweze kuendelea kutengenezwa na iweze kupitika.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya mchepuo kwenda Moshi kupitia Chekereni – Kahe – Mabogini - TPC kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Mji mdogo wa Mbalizi una kilomita 33 za vumbi. Je, ni lini Serikali itajenga barabara hizo kwa kiwango cha lami?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Suma Fyandomo juu ya barabara hizi za Mbalizi zenye urefu wa kilomita 33. Tutatuma timu ya kuweza kufanya tathmini kutoka Wakala wa barabara za Vijijini na Mijini (TATURA) ili kuona ni kiasi gani kinahitajika ili kujenga barabara hizi kwa kiwango cha lami. Baada ya kufanya tathmini hiyo tutaona ni kwa namna gani Serikali inaweza ikatafuta fedha kadri ya upatikanaji wake kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hizi.