Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kuhusu ujenzi wa barabara ya Mafinga hadi Mlimba?

Supplementary Question 1

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa barabara ya Mafinga - Kihansi inaungana na barabara ya Ifakara – Mlimba - Madeke mpaka Njombe Kibena junction, ninaishukuru Serikali kwa kuwa mwaka huu wa fedha bajeti ilitengwa ujenzi wa kiliometa 100 ianze kujengwa barabara hii ya Ifakara – Mlimba – Njombe, mpaka sasa taarifa nilizonazo mkataba umeshasainiwa ujenzi wa kilometa 62.5 uanze kujengwa. Swali langu dogo hapo ni kwamba; je, ni lini sasa mandarasi atakabidhiwa site na ujenzi uanze mara moja? (Makofi)

Kwa kuwa, barabara hii kwa mujibu wa bajeti ilitengwa kilometa 100 na kilometa 62.5 mkataba ulishasainiwa na kulikuwa na Lot I na Lot II. Lot zote mbili zilitangazwa mara moja. Swali langu la pili; je, hii Lot II kilometa 37.5 lini mkataba huu utasainiwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli Lot I kilometa 62.5 imeshasainiwa na Mkandarasi tayari alishapatikana na kazi hii imeshainiwa. Kinachosubiriwa sasa hivi, Mkandarasi baada ya kusaini anatakiwa atoe performance guarantee (dhamana ya utendaji) na lazima iwe imetolewa ndani ya siku 28. Kwa hiyo, tunaamini atakapokuwa amekamilisha takwa hilo la kisheria atakabidhiwa hiyo barabara ili aanze kufanya mobilization na inatakiwa ifanyike ndani ya siku 28.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa barabara hii ni kweli kama alivyosema ni kilometa 100 lot mbili, hizi kilometa 37.5 ambazo zimebaki, tayari kila kitu kimekamilika tunachosubiri ni kusaini tu, hii ni pamoja na barabara nyingine ambazo zilikuwa zinasubiria utaratibu wakuzisaini. Kwa hiyo, tunaandaa utaratibu ili barabara hizo ziweze kusainiwa halafu wakandarasi waanze kuzijenga. Ahsante. (Makofi)

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kuhusu ujenzi wa barabara ya Mafinga hadi Mlimba?

Supplementary Question 2

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Kwa kuwa, barabara ya Mlowo – Kamsamba iliingizwa kwenye bajeti kwa mwaka huu wa bajeti tulionao. Ningependa kujua ni lini Serikali itaanza kufanya kazi kwa vitendo, kuwaona wakandarasi site? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara zote ambazo tumezitengea kuanza utekelezaji kwa mwaka wa fedha huu wa 2023/2024 ndiyo kwanza taratibu zinaandaliwa ikiwa ni pamoja na kuaanda tender documents ili ziweze kutangazwa, wakandarasi waombe na waweze kufanyiwa taratibu zote za manunuzi. Kwa hiyo, tupo kwenye taratibu za awali kwa sababu ndiyo tunaanza utekelezaji wa bajeti wa mwaka huu wa fedha, ahsante. (Makofi)

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kuhusu ujenzi wa barabara ya Mafinga hadi Mlimba?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ziwa Nyasa ni karibu wiki moja limechafuka na akina mama wajawazito wameshindwa kabisa kuvuka kwenda kupata huduma pale Matema. Je, Waziri yuko tayari sasa kufuatana na mimi kuangalia jinsi gani barabara ya kutoka Matema kwenda Ikombe inavyosuasua?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza tutoe pole kwa changamoto ambayo inatokea katika Jimbo la Kyela. Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba yupo Mkandarasi ambaye alikuwa anasuasua na tayari tumeshamuagiza Meneja wa Mkoa wa Mbeya amsimamie ili kwanza aweze kukakamilisha eneo ambalo lilikuwa lina changamoto. Mimi nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya hapa tukubaliane tuende tukatembelee ili kuhakikisha kwamba kazi ambayo inafanyika iweze kukamilika. Nipo tayari kufuatana naye.

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kuhusu ujenzi wa barabara ya Mafinga hadi Mlimba?

Supplementary Question 4

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mtwara – Pachani – Luchili – Mkungu – Mtwara Matata – Ligera – Ligunga – Lusewa – Magazine – Lingusenguse – Nalasi – Mbesa mpaka Tunduru ina urefu wa kilometa 305, barabara hii ni ya kimkakati. Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tunatambua barabara hii ni kweli ni ya kimkakati na ya kiuchumi, tunachofanya sasa hivi, tulishakamilisha usanifu. Tulichoamua sasa hivi kutokana na urefu wa barabara na umuhimu wa hii barabara, tumeainisha maeneo yote ambayo yanasumbua pamoja na madaraja, tuyaimarishe na kujenga zege ama lami nyepesi ili barabara ile ipitike muda wote wakati huu tunatafuta fedha kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kuhusu ujenzi wa barabara ya Mafinga hadi Mlimba?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Kitonga ni barabara ambayo ni ya Kitaifa na imekuwa ikipitisha malori makubwa, inapopata ajali kidogo malori yamekuwa yakikwama kwa siku nzima au siku mbili, Serikali ilikuwa imetuahidi kujenga barabara mbadala ambayo itatokea Mahenge – Kudekwa kupita Wotalisoli mpaka Ilula.
Je, ni lini sasa ile ahadi ya Serikali itatekelezeka ili kuondoa changamoto kubwa katika Mlima Kitonga? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tuna kazi mbili ambazo tunazifanya, moja ni kuendelea kuipanua ile barabara ili iwe pana hasa hilo eneo la Kitonga, kuruhusu magari yaweze kupishana na kunapotokea changamoto tupate nafasi ya magari mengine kupita.

Mheshimiwa Spika, suala la pili ni kweli Serikali ina mpango wa kujenga bypass (njia ya mchepuko) kuchepusha kupita huo Mlima Kitonga kunapotokea changamoto na tumeunganisha nguvu kati ya TANROADS na TARURA ambao wanaendelea na usanifu wa hiyo barabara, baada ya hapo hiyo barabara itajengwa, ahsante.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kuhusu ujenzi wa barabara ya Mafinga hadi Mlimba?

Supplementary Question 6

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa.

Je, Serikali ina mkakati gani kukamilisha barabara ya Kiboroloni – Kichudini mpaka Kidia, kwa sababu barabara hii itakuwa inapandisha watalii kupitia Lango la Kidia. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara hii ya Kiboroloni sasa hivi inasimamiwa na TANROADS kupitia Meneja wa Mkoa na imepangiwa fedha ya maendeleo kwenda kwa awamu. Sasa pengine tutaangalia ukubwa wake ili kama inawezekana tuweze kuongeza fedha ili kipande kile kidogo kilichobaki kiweze kukamilika na ijengwe yote kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kuhusu ujenzi wa barabara ya Mafinga hadi Mlimba?

Supplementary Question 7

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Mwezi wa Sita tulisaini barabara ya Mafinga – Mgololo kupitia ule utaratibu wa EPC+F. Sasa wananchi wanapata shaka, wanasema mbona hawaoni mkandarasi, naomba Mheshimiwa Naibu Waziri awape comfort wananchi wa Mafinga katika barabara hiyo inayo - cut across Majimbo Matatu. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa miradi yote ya EPC+F Wakandarasi walishapatikana na walishasaini mikataba ikiwa ni pamoja na hiyo barabara ya Mafinga kwenda Mgololo. Kinachofanyika sasa hivi ni kwamba Wakandarasi wote wapo wanapita site, moja ikiwa ni kuangalia fidia, kuangalia sehemu watakazopata material, wapi watajenga kambi lakini pia hizi barabara kutokana na ukubwa wake kuzigawa kwenye lot kulingana na mazingira yake watakavyogawa Wakandarasi maana yake atakayejenga siyo Mkandarasi mmoja kulingana na ukubwa wa barabara.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo kuna barabara ambazo zitakuwa na Wakandarasi wawili, hadi wanne kulingana na ukubwa. Kwa hiyo, Wakandarasi wako wanapita na kupitia pia usanifu kwa sababu ni wao pia wanatakiwa wajiridhishe na usanifu uliofanyika kabla ya kuanza ujenzi. Kwa hiyo, niwahakikishie wananchi kwamba mpango huo unaendelea na watu wapo kazini, kitakachofanyika baada ya kukamilisha wataanza kuona mitambo ikiwa inawasili kwenye maeneo yao, ahsante. (Makofi)

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kuhusu ujenzi wa barabara ya Mafinga hadi Mlimba?

Supplementary Question 8

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Busisi – Sengerema hadi Igaka boarder ambayo inajengwa kwa barabara nne kwa kiwango cha lami. Lini kazi hiyo ya usanifu itaanza kufanyika maana yake toka imesemwa toka mwezi wa sita mpaka leo hatujamuona mkandarasi akifanya designing?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tukishafanya usanifu kinachofuata ni kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza huo ujenzi. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa Serikali imeshatoa commitment kwanza kufanya usanifu, basi hatua inayofuata itakuwa ni kujenga hiyo barabara kama ilivyosanifiwa. Kwa hiyo, mpango huo upo, hela zikishapatikana tutaanza kuijenga hiyo Barabara. Ahsante.

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kuhusu ujenzi wa barabara ya Mafinga hadi Mlimba?

Supplementary Question 9

MHE. BONNAH L. KAMOLI: Mheshimiwa Spika, barabara ya Bonyokwa – Kinyerezi walisema itaanza mwezi wa sita mpaka sasa hivi hajiaanza, je, ni lini itaanza hiyo barabara? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba hiyo barabara tumeitengea bajeti kwenye bajeti ya mwaka huo wa 2023/2024 na kama nilivyosema kwenye barabara zingine ambazo zimepewa fedha kwa mwaka huu taratibu zipo zinaandaliwa ili zianze kujengwa ikiwa ni pamoja na hiyo barabara ya Bonyoka – Kinyerezi. Ahsante.