Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza:- Je, lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Vijiji vya Msata, Kihangaiko na Pongwe Msungura kutokana na maeneo yao kuchukuliwa na Jeshi la Wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza mawali mawili madogo ya nyongeza. Kwanza niishukuru sana Serikali yetu ya Awamu ya Sita kwa kuonesha dhamira ya kushughulikia mgogoro huu ambao ulikuwa wa muda mrefu. Sasa kwa kuwa hatua ya kwanza ya kuanza kulipa malipo haya kwa Kitongoji cha Funta zaidi ya milioni 330 imeleta kama sintofahamu kwa wananchi wa Vitongoji vya Chokozeni na Kudikongo katika Kijiji cha Kihangaiko hicho hicho. Je, Serikali haioni ipo haja kwa vitongoji hivi viwili vya Kijiji kimoja cha Kihangaiko walipwe fidia yao kwa mwaka huu wa fedha unaoendelea?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa wapo baadhi ya wananchi waliotoa maeneo wa Vijiji vya Msata, Kihangaiko na Pongwe Msungura hawakupimiwa na kwa kuwa imeanza kulipa fidia. Je, Serikali inatoa tamko gani kwa wale wananchi ambao bado hawajapimiwa ili waweze kupata matumaini na waweze kuyaachia yale maeneo kuliko wanavyokwenda kufanya shughuli na wanakumbwa na matatizo makubwa? Ahsante sana.

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, kwa swali la kwanza ambalo ni kwamba kuna hawa ambao hawajalipwa, napenda tu kutoa rai kwa wenzetu ambao ni Halmashauri ya Chalinze kukamilisha taratibu na kuwasilisha jedwali ili taratibu ziendelee na ziweze kukamilika. Kama alivyosema ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba migogoro hii inakamilishwa na kama ambavyo Waheshimiwa Wabunge wengi wataona tulikuwa na migogoro 87 katika mpango wetu wa mwaka 2020 - 2023 na kati ya migogoro hiyo 87 migogoro 74 imekwishatatuliwa. Kwa hiyo hii 13 iliyosalia ni dhamira yetu kuhakikisha kwamba tunaikamilisha mwaka huu wa fedha kwani hata mpango tuliokuwa tumejiwekea kukamilisha mwaka 2023 umeshapita, tumeongeza mwaka mmoja.

Mheshimiwa Spika, kwa hao wengine ambao wamejitokeza, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaangalia kama hii migogoro mipya iko sehemu ya mpango wetu na kama haiko sehemu ya mpango wetu tutaona tunaiingiza namna gani. Jambo la kwanza ni muhimu tuende tukajiridhishe kwamba haya maeneo anayoyataja ni maeneo ambayo yapo katika maeneo ya vikosi vya Jeshi. Tutafanya hivyo Mheshimiwa Mbunge kwa kushirikiana na wewe.

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza:- Je, lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Vijiji vya Msata, Kihangaiko na Pongwe Msungura kutokana na maeneo yao kuchukuliwa na Jeshi la Wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa vile changamoto iliyoko katika Halmashauri ya Chalinze inafanana na changamoto iliyoko katika Halmashauri ya Bagamoyo katika Kata ya Mapinga katika eneo la Kiharaka. Je, Serikali lina mpango gani kulipa wananchi wa eneo la Kiharaka katika Kata ya Mapinga? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwishasema tunao mpango ambao umejumuisha migogoro mingi, kwa hiyo, kama hili eneo la Kiharaka ni sehemu ya mpango huu basi litakamilishwa katika mpango huu wa fedha, lakini kadri tulivyoendelea kutatua hii migogoro, migogoro mipya pia imekuwa ikijitokeza, kwa hiyo, kama huu ni mgogoro mpya tutaujumuisha katika mpango wetu baada ya kujiridhisha kwamba ni eneo ambalo lina mgogoro na Jeshi, ahsante.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza:- Je, lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Vijiji vya Msata, Kihangaiko na Pongwe Msungura kutokana na maeneo yao kuchukuliwa na Jeshi la Wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, moja kati ya maeneo ambayo yanaleta changamoto ni eneo la Kata ya Tambukareli ambapo ni eneo la Jeshi na kuna makaburi ya wananchi ambayo yapo kwenye eneo la Jeshi.

Je, Serikali mna mpango gani wa kwenda kufanya mazungumzo na wananchi ambao wamezika ndugu zao kwenye maeneo yale ili waweze kuendelea kufanya Ibada kwa marehemu waliotangulia mbele ya haki? (Makofi)

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa kuendelea kufuatilia suala hili kwa karibu sana. Hata kabla, huko nyuma tulishazungumza kuhusu suala hili, hili ni miongoni mwa maeneo ambayo yanafanyiwa kazi. Kwa hiyo, nikuhakikishie tu kwamba tutaendelea kulifanyia kazi ili tuweze kupata suluhu yake, ahsante. (Makofi)