Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza:- Je, lini Serikali itaiongezea fedha TARURA kwa ajili ya matengenezo ya barabara za Jimbo la Morogoro Kusini? (Makofi)

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali, pamoja na Serikali kuendelea kutenga fedha nyingi kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya barabara katika Jimbo la Morogoro Kusini, bado kuna uhitaji mkubwa wa fedha ambazo ningependa Serikali itenge.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kwenda na mimi akaangalie mazingira ya barabara katika Jimbo la Morogoro Kusini ili iwe rahisi kwa Serikali kuendelea kutenga fedha? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatambua kwamba Jimbo la Morogoro Kusini linahitaji fedha zaidi kwa ajili ya utekelezaji wa barabara hizi. Ndiyo maana katika kipindi cha miaka ya fedha mitatu mfululizo, Serikali imeendelea kuongeza bajeti ya barabara katika jimbo hili lakini pia katika majimbo yote.

Mheshimiwa Spika, namhakikishia kwamba nipo tayari kuambatana naye kwenda katika Jimbo la Morogoro Kusini. Tutakubaliana baada ya maswali haya ili tupange, baada ya Bunge tuweze kwenda na kuona hali ilivyo, lakini pia kushirikiana katika kuboresha huduma hiyo, ahsante. (Makofi)

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza:- Je, lini Serikali itaiongezea fedha TARURA kwa ajili ya matengenezo ya barabara za Jimbo la Morogoro Kusini? (Makofi)

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, barabara za Jimbo la Kilwa Kaskazini zilizo nyingi zina hali ya miinuko mikali pamoja na udongo korofi na zina hali mbaya sana. Je, Serikali ina mkakati gani wa barabara za aina hii ili kuboresha na kuhakikisha kwamba zinapitika muda wote wa mwaka? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya tathmini ya namna ya kufanya allocation ya fedha za barabara kwenye majimbo. Kwa sababu tunafahamu kwamba hali ya hewa inatofautiana, kuna majimbo yenye mvua nyingi kwa mwaka mzima. Kuna majimbo yenye milima na miteremko mikali, lakini kuna majimbo au wilaya ambazo zina udongo korofi kwa ujenzi wa barabara.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hata ule mgao wa fedha za Bajeti ya TARURA zinakwenda kwa kuzingatia vigezo hivyo, ukiwepo ukubwa lakini na hali ya kijiografia ya maeneo hayo. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, Serikali inatambua kwamba Kilwa Kusini na Kilwa kwa ujumla ina changamoto hiyo na ndiyo maana inaendelea kuongeza bajeti na tutaendelea kufanya hivyo kuhakikisha kwamba barabara hizi zinapitika vizuri zaidi. Ahsante. (Makofi)

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza:- Je, lini Serikali itaiongezea fedha TARURA kwa ajili ya matengenezo ya barabara za Jimbo la Morogoro Kusini? (Makofi)

Supplementary Question 3

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi, pamoja na maelezo aliyoyatoa sasa hivi, kulikuwa na ahadi ya Serikali kwamba majimbo yale ya mjini, ambayo yana mjini na vijijini yatapewa bajeti kubwa zaidi upande wa TARURA. Nini kauli ya Serikali kuhusu kutekeleza azma hiyo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli ilikuwa ni ahadi ya Serikali na niseme ahadi hiyo imeanza kutekelezwa. Kwa maana ya Manispaa na miji ambayo ina hali ya miji lakini pia vijijini, Serikali imeendelea kuongeza bajeti kuwezesha barabara za vijijini zijengwe vizuri, pia na barabara za mijini zijengwe vizuri.

Mheshimiwa Spika, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge likiwepo Jimbo la Njombe Mjini, tutahakikisha tunaendelea kuboresha utaratibu huu, ahsante. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza:- Je, lini Serikali itaiongezea fedha TARURA kwa ajili ya matengenezo ya barabara za Jimbo la Morogoro Kusini? (Makofi)

Supplementary Question 4

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, napenda kujua ni lini Serikali itajenga daraja la kuunganisha Kata ya Matongo na Kata ya Kibasuka, Nyarwana ili kusaidia mawasiliano wakati wa mvua? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba nitumie fursa hii kumwelekeza Meneja wa TARURA wa Mkoa wa Mara, lakini pia Wilaya ya Tarime kwenda kufanya tathmini ya gharama zinazohitajika katika ujenzi wa daraja hili la Matongo linalounganisha upande wa pili, ili sasa Serikali ifanye tathmini kuona kama liko ndani ya uwezo wa bajeti ya kila mwaka au linahitaji special bajeti ili tuweze kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo, ahsante. (Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza:- Je, lini Serikali itaiongezea fedha TARURA kwa ajili ya matengenezo ya barabara za Jimbo la Morogoro Kusini? (Makofi)

Supplementary Question 5

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ndiyo wilaya pekee yenye kilometa chache sana za barabara za changarawe na tuna chini ya kilometa nne tu za lami. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuiongezea wilaya hii fedha za TARURA ili kuongeza ufanisi wa ujenzi wa barabara hizo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli Jimbo la Liwale lina changamoto kubwa ya barabara. Katika bajeti zetu za miaka mitatu mfululizo, Mheshimiwa Kuchauka ni shahidi kwamba bajeti imeendelea kuongezeka, lakini najua bado haitoshelezi kutokana na ukubwa na changamoto kubwa ya barabara.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kuboresha suala la kuhakikisha kwamba barabara hizo zinatengewa fedha zaidi ili ziweze kupitika vizuri zaidi, ahsante. (Makofi)

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza:- Je, lini Serikali itaiongezea fedha TARURA kwa ajili ya matengenezo ya barabara za Jimbo la Morogoro Kusini? (Makofi)

Supplementary Question 6

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsante, Mji wa Iringa ni mji ambao barabara kubwa zote zinapita katikati ya mji; je, ni namna gani Serikali itatusaidia kwa dharura ili kupanua barabara za pembeni kwa kuwaongezea TARURA bajeti?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali lengo lake ni kuhahikisha kwamba barabara zetu zinapitika vizuri zaidi. Pia ni jukumu la halmashauri kuainisha maeneo ambayo wanadhani ni muhimu barabara zipanuliwe vizuri zaidi. Mameneja wa TARURA wa Mkoa na Wilaya wanatakiwa kufanya kazi hiyo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nitumie fursa hii kutoa wito kwa Meneja wa TARURA Mkoa wa Iringa, wa Wilaya ya Iringa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa, kuainisha barabara hizo, kutambua gharama zinazohitajika ili tuweze kuweka mpango kazi wa utekelezaji kwa awamu, ahsante. (Makofi)

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza:- Je, lini Serikali itaiongezea fedha TARURA kwa ajili ya matengenezo ya barabara za Jimbo la Morogoro Kusini? (Makofi)

Supplementary Question 7

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante, Halmashauri ya Wilaya ya Mbongwe imepakana na wilaya nne, lakini bajeti ya TARURA haitoshi na barabara zinahitaji kufunguliwa.

Je, ni lini Serikali Kuu itatoa pesa kwa TARURA ili kusudi njia zinazounganishwa na Wilaya ya Mbongwe ziweze kufunguliwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunatambua Wilaya ya Mbongwe inapakana na halmashauri almost nne. Kuna changamoto ya baadhi ya barabara ambazo zinaunganisha Halmashauri ya Mbongwe na halmashauri za jirani. Serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunaboresha ujenzi wa barabara hizo na tutaendelea kufanya hivyo. Ahsante. (Makofi)

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza:- Je, lini Serikali itaiongezea fedha TARURA kwa ajili ya matengenezo ya barabara za Jimbo la Morogoro Kusini? (Makofi)

Supplementary Question 8

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, kikao cha Mheshimiwa Waziri Mkuu na Mameneja wa TARURA, aliagiza Mikoa ya Kusini hususan Njombe, ikiwemo Wilaya ya Makete kuangaliwa kwa jicho la karibu kutokana na kwamba ni wilaya ambazo mvua zinanyesha kwa muda mrefu na Makete bajeti ya TARURA ni ndogo sana. Je, ni lini Serikali itaongeza fedha hizi na kuzingatia maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli yalikuwa ni maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, na sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI kazi yetu ni kutekeleza maelekezo hayo. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, tumeshafanya tathmini ya halmashauri zenye mvua nyingi, milima na aina ya udongo ikiwemo Halmashauri ya Makete na bajeti ya barabara katika Halamashauri ya Wilaya ya Makete itaendelea kuongezwa. Ahsante. (Makofi)