Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 57 2023-09-04

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza:-

Je, lini Serikali itaiongezea fedha TARURA kwa ajili ya matengenezo ya barabara za Jimbo la Morogoro Kusini? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. NDUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Edward Kalogeris, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TARURA imeendelea kuongeza bajeti kwa ajili ya ujenzi, ukarabati na matengenezo ya miundombinu ya barabara katika Jimbo la Morogoro Kusini. Bajeti ya utekelezaji wa miundombinu ya barabara imeongezeka kutoka kilometa 51.5 kwa shilingi milioni 660.95 kwa mwaka wa fedha 2020/2021 hadi kilometa 65.90 kwa shilingi bilioni 1.88 kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2023/2024 jumla ya shilingi bilioni 2.2 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi, ukarabati na matengenezo ya miundombinu ya barabara yenye urefu wa kilometa 85.9. Serikali itaendelea kuongeza bajeti kwa ajili ya uimarishaji wa miundombinu ya barabara katika Jimbo la Morogoro Kusini, ahsante. (Makofi)