Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA K.n.y. MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isiwekeze fedha Kiwanda cha Viuadudu Kibaha ili kutokomeza malaria nchini?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Waziri, je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha Buy Lava Off Taking Agreement unasainiwa ili kuiwezesha Wizara ya Afya kununua dawa zinazotengenezwa na kiwanda hiki ili kutokomeza malaria nchini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, ninataka kujua sasa ni lini kiwanda hiki kitalipa deni linalodaiwa na TANESCO ili waweze kurudishiwa umeme na kuhakikisha kazi ya uzalishaji wa dawa ya viuadudu inaendelea kwa kasi ile ile? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri wa Afya pamoja na Waziri wa Viwanda wameunda taskforce ambayo inashungulikia kiwanda hiki kiweze kupata ithibati na hiyo mikataba kuweza kusainiwa. Wiki ijayo tunakutana kwa ajili ya kuona ni namna gani tunaweza kwenda mbele na tatizo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia swali lako la pili la suala la umeme nafikiri mojawapo ya ajenda kwenye hicho kikao itakuwa pamoja na hili suala la umeme tutalitatua kwa pamoja. Nataka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge hili suala litashughulikiwa na litapata suluhu muda si mrefu. (Makofi)

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA K.n.y. MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isiwekeze fedha Kiwanda cha Viuadudu Kibaha ili kutokomeza malaria nchini?

Supplementary Question 2

MHE. STELLA A. IKUPA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, ili kuendelea kutokemeza malaria nchini, pamoja na majibu mazuri yaliyotolewa hapa, Serikali inaonaje ikajielekeza pia kutuhamasisha sisi wananchi kufanya fumigation kwenye makazi yetu? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza swali lake hilo liko straight, kwanza nimuombe awe balozi wa kwanza na niwaombe Wabunge mliopo hapa mtusaidie kuhamasisha na tunalichukua kama alivyolisema, tunaenda kutekeleza. (Makofi)

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA K.n.y. MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isiwekeze fedha Kiwanda cha Viuadudu Kibaha ili kutokomeza malaria nchini?

Supplementary Question 3

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi, naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, je, Serikali ina mpango gani wa kutambua, kwa sababu hii teknolojia ya viuadudu ni teknolojia ya kuangamiza mbu. Mbu ni kiumbe aliyeumbwa na Mungu kuishi duniani.

Je, Serikali imefanya mkakati gani kwamba teknolojia hii ikitamalaki mbu wote watakuwa wamekwisha yaani hatutakuwa na mbu. Je, Serikali imeshafanya utafiti kutambua umuhimu wa mbu kuwepo duniani?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli anachosema Mheshimiwa Nyongo, anazungumzia kweli unapomuondoa kiumbe yoyote ndani ya ikolojia kuna madhara yake kwenye ikolojia. Kwa sababu sehemu mbalimbali duniani wamekuwa wakifanya hilo na wakatokomeza mbu wanaoeneza malaria na haijawahi kutokea tatizo kwenye ikolojia ambalo limeweza kuleta madhara ya kibinadamu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri aendelee kuiamini hii sayansi inayoenda kutumika kwa sababu moja, sisi tunaenda kumtegea mbu pale ambapo anazaliwa kwa maana ya kumuondoa pale ambapo anazaliana, lakini anapokosekana hapa ndiyo tunatumia alichosema dada yangu Mheshimiwa Ikupa kwa maana ya kunyunyuzia.

Mheshimiwa Naibu Spika, anaposhindikana eneo hilo tunatumia net, tunaenda kutumia hizo mbinu zote. Nataka kumhakikishia kwamba kitakachoenda, ndiyo maana tunataka ipate ithibati kupitia Shirika la Afya Duniani kwa maana ya WHO ili kuhakikisha hayo mambo yote unayoyasema ya ikolojia na mambo mengine yamezingatiwa, ahsante.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA K.n.y. MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isiwekeze fedha Kiwanda cha Viuadudu Kibaha ili kutokomeza malaria nchini?

Supplementary Question 4

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, suala hili ni suala la muda mrefu kiwanda hiki kutonunuliwa dawa hizi. Serikali imekuwa ikiziomba halmashauri zetu ziweze kununua dawa hizi ili kutokomeza malaria kwenye Majimbo na Mikoa yetu ya Tanzania.

Je, ninyi kama Wizara mna mpango gani wa kutoa waraka maaalum ili angalau halmashauri zetu ziweze kununua hizi dawa na tuweze kutokomeza malaria nchini? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa maana anaonekana kwamba anatamani hili litokee kwa nguvu. Kwa hiyo, tayari ni balozi wetu. Ninachosema ni juzi Waziri wa TAMISEMI alikuwa na Wakuu wote wa Wilaya, Wakurugenzi wote na Wakuu wa Mikoa. Mojawapo ya makubaliano ni kwamba wahakikishe wameweka fedha kwa ajili ya afua ya lishe, pia wahakikishe wameweka fedha kwa ajili ya kununua viuddudu wa kutokomeza malaria.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hilo linafanyika na la kuandika waraka tutaenda kushirikiana na wenzetu wa TAMISEMI tutaandika waraka maalumu kuhakikisha mambo haya yanatokomezwa.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA K.n.y. MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isiwekeze fedha Kiwanda cha Viuadudu Kibaha ili kutokomeza malaria nchini?

Supplementary Question 5

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nilikuwa kwenye swali hilo hilo. Mlihakikisha kwamba Halmashauri zetu zinanunua dawa kutoka kwenye hicho kiwanda, lakini naona NBS walipojenga hiki kiwanda ilikuwa ni makusudi maalum kabisa kwamba fedha hizi zirudi ndani ya shirika lile.

Je, sasa hamuoni ipo haja Serikali itoe mamlaka zaidi ili tuweze kununua dawa kutoka kwenye Manispaa zetu kutoka kwenye hiki kiwanda ili kiwanda hiki kiendelee kujiendesha kwa sababu sasa hivi naona kama kiwanda chenyewe hakipo tena? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, ukiona tumeomba shilingi bilioni 129.1 kwa maana tunaomba fedha maalumu kutoka Wizara ya Fedha, hiki ni kikao ambacho Waziri Mkuu mwenyewe amekisimamia na ameki-push ili haya mambo yatokee.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano, alikaa mwenyewe kikao na kuelekeza tulifanye hili na pia kwa maana ya ushauri wenu pia uandikwe waraka kuhakikisha kwenye CCHP za halmashauri inawekwa bajeti kwa ajili hiyo. Tukifanya hayo yote tutaenda kufakinikiwa.