Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 4 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 53 2023-09-01

Name

Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA K.n.y. MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza: -

Je, kwa nini Serikali isiwekeze fedha Kiwanda cha Viuadudu Kibaha ili kutokomeza malaria nchini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali na Mheshimiwa Rose Cyprian Tweve, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mhemishimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha mwaka 2017 hadi 2023, Serikali imenunua viuadudu vyenye thamani ya shilingi bilioni 5.9 na kutumika katika ngazi ya halmashauri.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuhakikisha uhakika wa upatikanaji wa viuadudu kutoka Kiwanda cha Kibaha, kwa kipindi cha mwaka 2024 - 2026, Wizara ya Afya imeomba kupatiwa jumla ya shilingi bilioni 129.1 kwa ajili ya utekelezaji wa afua ya unyunyiziaji wa viuadudu ili kuangamiza viluilui vya mbu kwenye mazalia ili kufikia lengo la kutokomeza malaria ifikapo mwaka 2030.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Afya inashirikiana na Shirika la Taifa la Maendeleo ya Viwanda kuhakikisha kiwanda kinapata ithibati kutoka Shirika la Afya Duniani ili kuongeza wigo wa upatikanaji wa fedha za kutekeleza afua hii kutoka kwa wadau mbalimbali wa mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.