Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kumaliza upungufu wa madawa na vifaa tiba katika hospitali zetu nchini?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa takwimu za Bohari ya Madawa, sasa hivi upatikanaji wa dawa ni asilimia zaidi ya 80, lakini ukienda kwenye uhalisia, hicho kitu ni tofauti kabisa. Kumekuwa na shida kubwa ya dawa sijui tatizo ni nini? Hilo la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili ni kwamba, sasa kumekuwa na tatizo sugu kabisa kwenye hospitali zetu nyingi; wagonjwa kila wanapokuwa wameandikiwa dawa nyingi huwa wanaambiwa wakanunue kwenye maduka ya watu binafsi: Je, Serikali ina mpango gani wakutatua tatizo hili la wagonjwa kila mala kuandikiwa kwenda kununua dawa katika maduka ya watu binafsi? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza amesema kwenye takwimu za Bohari ya Dawa upatikanaji wa dawa ni asilimia 80, lakini ukienda kwenye uhalisia unakuta kuna jambo tofauti. Labda nimwambie Mheshimiwa Mbunge, ni kweli kwamba ukiangalia kwenye hospitali zetu za Taifa mpaka hospitali zetu za mikoa, upatikanaji wa dawa ni asilimia 97, kwa sababu wanatumia dawa zinazotoka Bohari ya Dawa na pia wanatumia mapato ya ndani kununua dawa wenyewe. Kwa hiyo, asilimia yao ni kubwa kuliko hata ile ambayo ipo Bohari ya Dawa. Pia kwenye hospitali zetu za wilaya, ni kweli kwamba sasa upatikanaji wa dawa kwa sasa ni asilimia 68, maana yake kuna asilimia 32 ya watu ambao bado wanakosa dawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge ni shahidi kwamba ukilinganisha mwaka jana 2022 na sasa kuna ongezeko la upatikanaji wa dawa. Kama ambavyo sasa MSD inaenda kupata mtaji kutoka Serikalini ili waweze kununua dawa mapema, sasa hilo tatizo litaisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Mheshimiwa Mbunge amesema kuna tatizo sugu la wananchi kukosa dawa na wanatakiwa kununua kwenye maduka ya watu binafsi. Hilo hilo linajibu, kwa sababu kama ndani ya hospitali zetu za wilaya na vituo vyetu kwenye hospitali za mikoa kwenda Taifa ni asilimia 97, maana yake kuna upungufu wa asilimia tatu. Ukija kwenye hospitali zetu za wilaya kushuka chini asilimia 32, kwa hiyo, ni lazima watanunua.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumwambia Mheshimiwa Mbunge, kwa mkakati ambao umewekwa hapa na Serikali kwa maana ya kutoa mtaji MSD, tutaenda kutatua hilo tatizo kama ambavyo anategemea litatuliwe. (Makofi)

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kumaliza upungufu wa madawa na vifaa tiba katika hospitali zetu nchini?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Hospitali ya Rufaa Njombe, tunaishukuru Serikali kwanza kwa kuleta vifaa tiba na kuweza kuiboresha, lakini bado wananchi katika Mkoa wa Njombe wana matatizo makubwa sana ya uhitaji wa kusafishwa damu na bado inawabidi wasafiri: Ni lini Serikali italeta mashine ya kusaidia kusafisha damu kwa wagonjwa wa figo katika Hospitari ya Rufaa ya Njombe?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimemsikiliza, kama vile anasema suala la upatikanaji wa damu, lakini nilichomwelewa anamaanisha kusafisha figo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeagiza hospitali zote za mikoa, na vifaa vipo kwa ajili ya kuweka majengo ya kusafisha damu. Kwa sababu hospitali yetu ni mpya, namwomba Mheshimiwa Mbunge tufanye mawasiliano tujue jengo kwa ajili ya kusafisha damu, kwa maana ya kutibu wagonjwa wa figo, lipo kwenye hatua gani ya ujenzi ili vifaa viweze kwenda kwa ajili ya kutatua tatizo hilo.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kumaliza upungufu wa madawa na vifaa tiba katika hospitali zetu nchini?

Supplementary Question 3

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Hospitali ya Selian imekuwa ni hospitali ambayo inatoa msaada mkubwa sana kwa wakazi wa Arusha, lakini hospitali hii imekuwa inapitia changamoto nyingi: Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuisaidia hospitali hii ya Selian kama ambavyo imekuwa ikisaidia hospitali nyingine? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Hospitali ya Selian kwa maana ya ALMC inapitia katika changamoto ambapo tumeona wanafika mahali wanakaa mpaka miezi minne hawajalipa mishahara, na walishaleta maombi yao Serikalini kwa ajili ya kusaidiwa kwenye baadhi ya mambo ili waweze kujikwamua kwenye hali hiyo. Serikali imeshaunda timu, na timu imeenda kwenye hospitali hiyo, wamefanya uchunguzi ili kujua ni matatizo gani ambayo yanaikumba hospitali hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeshayaona matatizo, kuna mengine tumewaambia warekebishe na watupe Subira kwani kuna mchakato unaendelea ndani ya Wizara zetu ili tujue tutafanya nini. (Makofi)

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kumaliza upungufu wa madawa na vifaa tiba katika hospitali zetu nchini?

Supplementary Question 4

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa Halmashauri ya Msalala tumekamirisha ujenzi wa vituo vya afya viwili na zahanati 24: Nini mkakati wa dharura wa Serikali wa kuhakikisha kwamba wanapeleka vifaa tiba ili zahanati hizi na vituo vya afya vianze kufanya kazi haraka iwezekanavyo? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi na Mheshimiwa Mbunge, tumetembelea vituo hivyo na nimeona kweli kuna tatizo hilo. Namwomba Mheshimiwa Mbunge aje tukae pamoja, tumpigie DMO wake ili aweze kutuma list ya vifaa ambavyo tulikuwa tumeona havipo tupeleke MSD ili aweze kupata vifaa. (Makofi)

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kumaliza upungufu wa madawa na vifaa tiba katika hospitali zetu nchini?

Supplementary Question 5

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tatizo la madawa nchini linaweza kwisha iwapo tu Serikali itaamua kutoa fedha za mtaji ambazo Bohari Kuu ya Dawa Nchini (MSD) wameomba. Wameomba takribani shilingi bilioni 200.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, anaweza kutuhakikishia Wabunge kwamba Serikali ipo tayari kutoa hizo fedha za mtaji ili kumaliza tatizo la usambazaji wa dawa hapa nchini kwenye vituo vyetu vya afya na zahanati?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, hilo lilikuwa ni mjadala mkubwa sana hapa ndani ya Bunge wakati wa bajeti. Nawashukuru ninyi Wabunge kwamba mlilipitisha hilo na Serikali ipo tayari, ndiyo maana wakati wa bajeti, Waziri wa Afya na Waziri wa Fedha walikiri kwamba hilo litaenda kufanyiwa kazi.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kumaliza upungufu wa madawa na vifaa tiba katika hospitali zetu nchini?

Supplementary Question 6

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Changamoto hii ya ukosefu wa dawa imetugharimu sana kwa wananchi: Je, Serikali haioni kuwa sasa ni wakati muafaka wa kuweka alama dawa za Serikali ili kudhibiti upotevu? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kuweka alama limekuwa ni endelevu na dawa zote za MSD zimekuwa na alama. Ninachoweza kumwomba Mheshimiwa Mbunge, kwenye Baraza la Madiwani suala la dawa na vifaa tiba liwe ni ajenda ya kudumu. Pia nawaomba Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya hilo liwe ni ajenda ya kudumu, kwa sababu ni ukweli kwamba upungufu mkubwa unasababishwa na matumizi mabaya ya fedha yanayopatikana baada ya kuuza huduma na dawa zenyewe, na pia baadhi ya dawa kuibiwa kwenye vituo vyetu.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kumaliza upungufu wa madawa na vifaa tiba katika hospitali zetu nchini?

Supplementary Question 7

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza. Kumekuwa na changamoto katika maeneo mbalimbali nchini. Aidha, hospitali ina vifaa tiba vya kutosha, haina wataalam; au ina wataalam, haina vifaa tiba: Serikali haioni haja sasa yakupeleka hivyo vikaenda sambamba ili kutumia fedha hizi vizuri za walipa kodi? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Mbunge, kwa sababu anakubaliana kwamba kuna wakati watumishi wamekuwepo lakini kunakuwa nashida ya vifaa tiba na wakati mwengine kunakuwepo na vifaa tiba, lakini hakuna watumishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, na kama kuna hilo tatizo kwenye jimbo lake la hiyo irregularity, aniletee tuone jinsi ya kulitatua kwa pamoja.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kumaliza upungufu wa madawa na vifaa tiba katika hospitali zetu nchini?

Supplementary Question 8

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Tumejenga vituo vya afya viwili vya Hydom na Eshkesh, havina vifaa tiba na mmetuletea madaktari: Je, lini mnapeleka vifaa tiba ili wananchi wapate huduma ya utabibu?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimeshasema hapa, Rais wetu ameshatoa kwa ajili ya kununua vifaa tiba kwa vituo vyote ambavyo vimeisha. Namwomba Mheshimiwa Mbunge, nikitoka hapa, tutakaa pamoja naye tujue ni vifaa gani vinahitajika ili tuweze kuweka utaratibu wa kuvipeleka kwenye eneo lake. (Makofi)

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kumaliza upungufu wa madawa na vifaa tiba katika hospitali zetu nchini?

Supplementary Question 9

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru ina uhaba mkubwa wa madaktari: Je, Serikali ina mpango gani kuongeza madaktari katika hospitali hii ambayo inahudumia zaidi ya mikoa mitatu? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru nafikiri anachomaanisha Mheshimiwa Mbunge, ni upungufu wa madaktari bingwa. Ni kweli kwenye hospitali yetu ya Mount Meru na siyo Mount Meru peke yake, hospitali nyingi kuna upungufu wa madaktari bingwa. Ndiyo maana Rais wetu ametoa shilingi bilioni tisa kwa ajili ya kusomesha madaktari bingwa. Mmesikia Dkt. Samia Suluhu Hassan Scholarship ambayo inaendelea na tunaendelea namna hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mount Meru wana madaktari ambao wapo shuleni ambao pia wamesomeshwa kuanzia miaka miwili iliyopita, kwa maana hao wakimaliza shule, upungufu huo ambao upo Mount Meru utapungua.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kumaliza upungufu wa madawa na vifaa tiba katika hospitali zetu nchini?

Supplementary Question 10

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya cha Mkansila, tunashukuru Serikali ilituletea fedha na Kituo cha Afya cha Masamakati, wewe mwenyewe Mheshimiwa Naibu Waziri, ulituhamasisha pale tukajenga kwa nguvu za wananchi na fedha ya Halmashauri: Je, ni lini Serikali italeta fedha ya kumalizia vituo hivi vya afya viwili?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tumekwenda na Mheshimiwa Mbunge, tukakuta wananchi wanaohitaji zahanati, tuliwaomba na tukawahamasisha pamoja na yeye ili waweze kuanza wakati Serikali inakuja nyuma. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge hapa, kabla ya mwezi wa Tatu mwakani 2023, kazi hiyo itakuwa imeisha. (Makofi)

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kumaliza upungufu wa madawa na vifaa tiba katika hospitali zetu nchini?

Supplementary Question 11

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kituo cha Afya Mkoga, kimejengwa kwa nguvu za wananchi na Mfuko wa Jimbo, tumefikia hatua ya boma: Je, Serikali inawezaje kutusaidia ili tumalizie kwa sababu tunahitaji sana huduma kwa eneo lile? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimwambie Mheshimiwa Mbunge, kama ambavyo Serikali imekuwa ikitoa fedha shilingi milioni hamsini hamsini kwa ajili ya kumalizia vituo kama hivyo, navyo tutaenda kuviangalia na tutahakikisha na kituo chake kinakuwepo kwenye orodha ya vituo ambavyo vitamaliziwa.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kumaliza upungufu wa madawa na vifaa tiba katika hospitali zetu nchini?

Supplementary Question 12

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni je, Serikali inatoa ushirikiano gani kwa vituo vya afya vinavyomilikiwa na sekta binafsi hususan Makanisa ili viweze kutoa huduma kwa wananchi wanaotegemea sana hivi vituo kwa bei nafuu? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwepo na utaratibu wa Serikali kushirikiana na hivyo vituo kwa mikataba maalum. Kama Mheshimiwa Mbunge anakumbuka hata kwenye jimbo lake kuna kituo ambacho kuna ushirikiano kama huo, naomba kama kuna Kituo ambacho amekiona kinategemewa sana na wananchi na vituo vingine vipo mbali na anahitaji hilo, angeleta ili kupita kwenye mchakato ikionekana inafaa na ikikidhi vigezo, basi Serikali itatafakari la kufanya. (Makofi)