Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 4 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 52 2023-09-01

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kumaliza upungufu wa madawa na vifaa tiba katika hospitali zetu nchini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuboresha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba katika hospitali zetu nchini kwa kutekeleza yafuatayo: -

(1) Kuipatia mtaji Bohari ya Dawa kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ili kuwa na bidhaa za afya muda wote;

(2) Serikali kutoa fedha za ununuzi wa bidhaa za afya kila mwezi kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma za afya vya Serikali;

(3) Kuhakikisha suala la usimamizi wa bidhaa za afya linakuwa sehemu ya ajenda ya kudumu ya Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya na Mikoa;

(4) Kuwasimamia watoa huduma katika vituo vya kutolea huduma za afya ili kuweza kukadiria makadirio sahihi (forecasting); na

(5) Vituo vya kutolea huduma za afya kutumia fedha zinazotokana na malipo ya huduma na dawa kununua bidhaa za afya kuliko kutegemea fedha zinazotolewa na Serikali pekee.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.