Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha bei ya Zao la Mkonge haitetereki?

Supplementary Question 1

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu ya Serikali, nina maswali madogo mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; moja ya njia ya kutoa bei nzuri isiyotetereka ya zao la mkonge ni kuwa na nyuzi bora, kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri. Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza ahadi yake ya kununua mashine za kuchakata mkonge, ili mazao ya mkonge, nyuzi zinazochakatwa ziwe na ubora ukizingatia kwamba, tuna changamoto kubwa ya uhaba wa mashine?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; katika kuimarisha soko la ndani, kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri, Serikali ilitoa agizo la kuzuia uingizaji wa kamba na nyuzi za plastic, lakini mpaka leo hali bado sio nzuri. Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya kudhibiti uingizaji wa nyuzi na kamba za plastic kwenye nchi yetu?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya maeneo ambayo tunatilia mkazo ni kuwa na teknolojia sahihi ya kuzalisha bidhaa mbalimbali, ikiwemo nyuzi zinazotokana na mkonge. Katika jitihada hizo tumeshaweka bajeti kwa ajili ya kununua mashine hizo za kisasa ambazo ziliahidiwa, lakini zaidi kupitia taasisi zetu za ubunifu, TEMDO, kuna mashine inaandaliwa ambayo nayo itasaidia kuchakata mkonge, ili kupata nyuzi bora na zenye tija kwa ajili ya kuhakikisha tunapunguza uingizaji wa nyuzi mbadala za plastic kutoka nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kuzuia uingizaji wa nyuzi za plastic kama unavyojua ni kweli, bado mahitaji ni makubwa zaidi ya bidhaa hii kuliko uwezo wa kuzalisha wa ndani, kadri tunavyoendelea kuimarisha uzalishaji wa nyuzi za mkonge naamini tutapunguza hilo gap na pale tutakapokuwa tumejitosheleza, maana yake hii marufuku itaisha ili kuhakikisha hatuagizi tena nyuzi za plastic kutoka nje, nakushukuru. (Makofi)

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha bei ya Zao la Mkonge haitetereki?

Supplementary Question 2

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha bei ya zao la kahawa kwa wakulima wanaolima kahawa aina ya Arabika na Robusta? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Prof. Ndakidemi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli moja ya maeneo ambayo Serikali inaangalia kwa ukaribu sana ni kuona namna gani tunaboresha bei ya mazao ya kilimo ikiwemo Kahawa katika nchi hii. Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, tunaendelea kuongeza uwekezaji. Mosi, uwekezaji wa viwanda vya kuchakata zao la Kahawa. Pili, kuona tunafungua masoko ili wananchi hawa ambao wanazalisha, hata wale ambao hawajaongeza thamani waweze kuuza popote. Kwa hiyo, maana yake kupitia hiyo najua bei yake itaongezeka kwa sababu mahitaji yatakuwa makubwa kwa hiyo bei nayo itapanda. Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha bei ya Zao la Mkonge haitetereki?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Iringa ni kati ya Mikoa iliyohamasisha kulima kwa wingi zao la parachichi, changamoto inayowakabili ni bei kubwa sana ya miche ya mbegu. Je, ni lini Serikali itaona umuhimu hata kuwapatia miche ya ruzuku ili wananchi waweze kulima kwa wingi zaidi? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ritta Kabati, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali yetu ya Awamu ya Sita kama nilivyosema, chini ya Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeongeza fedha nyingi sana kwenye sekta hii ya kilimo na ninyi ni mashahidi kutoka billioni 200 mpaka karibu trilioni moja sasa. Moja ya maeneo ambayo yameangaliwa ni kuongeza ruzuku kwenye uzalishaji wa miche ya mazao mbalimbali ikiwemo parachichi. Hii tayari tumeshaweka na kule Iringa tayari pale Kilolo kuna miche ambayo inazalishwa kwa ajili ya ruzuku.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni muda tu kwamba wakulima wawasiliane na Idara ya Kilimo katika Mkoa wa Iringa ili waweze kupata miche ya ruzuku kwa ajili ya kupanda zao hili la parachichi. Nakushukuru. (Makofi)