Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 4 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 48 2023-09-01

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:-

Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha bei ya Zao la Mkonge haitetereki?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha bei ya zao la mkonge haitetereki, Wizara ya Kilimo kupitia Bodi ya Mkonge imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kuimarisha soko la ndani kwa kuongeza matumizi ya ndani katika kutengeneza bidhaa zilizoongezwa thamani kama vile kamba, mazulia, magunia, mapambo na bidhaa za ufumaji na kupunguza matumizi ya bidhaa kutoka nje kama uagizaji wa kamba za plastiki, mazulia na vifungashio.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara inaendelea kutenga bajeti kila mwaka kuanzia mwaka wa fedha 2022/2023 kwa ajili ya kununua mashine mpya za kuchakata (makorona) ili kuhakikisha kuwa, ubora wa mkonge unaochakatwa unakidhi matakwa na viwango vya soko la ndani na soko la kimataifa na hivyo kuimarisha bei ya zao hilo, nakushukuru sana.