Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha mafuta ya kula yanazalishwa kwa wingi nchini?

Supplementary Question 1

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina swali moja la nyongeza. Je, Serikali haioni umefikia wakati wa kuhamasisha wawekezaji wa ndani ili kusudi waweze kuzalisha mafuta yanayotokana na alizeti, ufuta, karanga, pamba, pamoja na mafuta yanayotokana na mifugo?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Ni kweli moja ya maeneo ambayo Serikali imeweka kipaumbele ni kuhamasisha uzalishaji wa mafuta kwa wazalishaji wa ndani, pamoja na kukaribisha wawekezaji kutoka nje, lakini mkakati mkubwa ni kwa wazalishaji wa ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, hili tunalifanya kupitia, mosi kama nilivyosema, kuwawezesha wakulima ili kulima mbegu zenye ubora na zenye tija. Pili, tunatengeneza teknolojia rahisi, viwanda vidogovidogo ambavyo vitapelekea wananchi hawa wazalishaji wa ndani kuzalisha mafuta mengi, lakini yenye ubora kwa sababu, changamoto hapa si tu upatikanaji wa mafuta, lakini pia tunataka mafuta yenye ubora ambayo yatakuwa hayana athari hasi kwa walaji. Kwa hiyo, tunaendelea kuhakikisha tunawezesha teknolojia rahisi ili kuzalisha zaidi mafuta ya kula hapa nchini.