Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 4 Industries and Trade Wizara ya Viwanda na Biashara 47 2023-09-01

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ aliuliza:-

Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha mafuta ya kula yanazalishwa kwa wingi nchini?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Fatma Hassan Toufiq, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeendelea kutekeleza mkakati wa kuendeleza Sekta Ndogo ya Alizeti na Chikichi ambayo ndiyo mazao makubwa yanayoweza kuzalisha kwa tija mafuta ya kula hapa nchini kwa sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika utekelezaji wa mkakati huo, viwanda vipya, kama Qstec na Jeolong vimeanzishwa. Upanuzi wa viwanda kama Mount Meru Millers, lakini pia, Serikali imeongeza nguvu katika taasisi za utafiti wa mbegu na hivyo kuongeza uzalishaji wa mbegu bora za alizeti na michikichi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Serikali inaelekeza nguvu zaidi kwenye kilimo cha kuzalisha mbegu bora, ili kukidhi mahitaji ya malighafi katika viwanda vyetu vya ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.