Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:- Je, ni miradi mingapi ya kimkakati imejengwa katika Wilaya ya Ileje?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na ucheleweshaji wa ukamilishaji wa miradi mingi ya kimkakati ambayo inakuwa imeandaliwa na Serikali. Swali la kwanza; nataka kufahamu ni nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha miradi hii ya kimkakati inaisha kwa wakati? Mfano mzuri ni Mradi wa Chumvi, Momba, mpaka leo haupelekewi fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; nataka pia, kufahamu, kwa kuwa, kumekuwa na miradi mingi ambayo inaibuliwa ambayo inatumia fedha nyingi za Serikali na haiishi kwa wakati na mingine imekuwa na poor designing na allocation ya miradi kwa hiyo, pesa nyingi zinaenda zinakuwa hazileti tija kwa wakati. Ni nini mkakati wa Serikali wa kupunguza hasara inayotokana na miradi hiyo ambayo inakuwa imebuniwa chini ya kiwango? Ahsante.

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Miradi mingi inayotekelezwa na Serikali ni kweli mingine inaweza kuwa na changamoto katika utekelezaji wake kutokana na sababu mbalimbali, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, miradi ambayo imeshawekewa mikakati maalum na ikatengewa fedha kwa wakati husika, tunatekeleza kwa wakati. Pale kunapokuwa na changamoto basi zinakuwa ni zile ambazo ziko nje ya uwezo ambao tumeupanga.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, Mbunge ametoa mfano wa Mradi wa Chumvi, Momba ni kwamba, huu ulibuniwa na Halmashauri, lakini na sisi kama Serikali Kuu tutaweka fedha hapo kama tulivyosema hapo awali, ili waweze kutekeleza mradi huo, lakini kwenye miradi mingine ambayo inatekelezwa kwa muda mrefu, Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeshatoa maelekezo kwamba, miradi ambayo imewekwa kwenye mipango lazima tuikamilishe kulingana na wakati na fedha nyingi zitatolewa kadiri ambavyo Serikali inapata, ili kuhakikisha tunaondokana na ucheleweshaji katika miradi husika, nakushukuru.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:- Je, ni miradi mingapi ya kimkakati imejengwa katika Wilaya ya Ileje?

Supplementary Question 2

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Halmashauri ya Mji wa Mafinga imetenga eneo la ekari 750 kwa ajili ya Industrial Park ili tuweze kuwa soko la kimataifa la mazao ya misitu; je, Serikali iko tayari kushirikiana na sisi kupitia EPZA kufanikisha ndoto hiyo ambayo itakuwa ni chanzo cha mapato na chanzo cha ajira?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Chumi, lakini Halmashauri ya Mafinga kwa kutenga maeneo haya ambayo ni mumhimu sana kwa ajili ya uwekezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tunathamini na tutahakikisha tunapeleka wawekezaji, lakini pia kusajili eneo hili chini ya uwekezaji, EPZA, ili mazao au bidhaa zinazozalishwa pale ziweze kuuzwa nje, lakini na ndani ya nchi katika kujiletea maendeleo katika Halmashauri ya Mafinga, lakini nchi kwa ujumla, nakushukuru sana.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:- Je, ni miradi mingapi ya kimkakati imejengwa katika Wilaya ya Ileje?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Kuelekea mwishoni mwa mwaka jana Serikali ilichukua hatua za kuweka mipaka ya kudumu eneo linalozunguka Uwanja wa Kimataifa wa KIA kwa lengo la kuweka miradi ya kimkakati. Je, ni miradi mingapi ya kimkakati na ni ya namna gani ambayo itajengwa kwenye eneo lile kwa sababu imechukua eneo kubwa sana takribani square kilometer 110? Ahsante.

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Ni kweli lengo la Serikali ya Awamu ya Sita, kama nilivyosema chini ya Rais wetu mpendwa, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ni kuona tunaongeza uwekezaji, kuvutia mitaji katika uwekezaji, uwekezaji wa ndani, lakini pia uwekezaji kutoka nje. Jambo hili linataka maeneo mahususi ambayo yameshaandaliwa tayari ili kupunguza ukiritimba na urasimu wa kutokupata maeneo ya uwekezaji kwa wawekezaji katika maeneo mengi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, eneo hili la KIA linafanyiwa tathmini ili kuona miradi mahususi ya kimkakati ambayo itawekezwa katika eneo hili ambalo mwanzoni lilikuwa kidogo na changamoto ya kuingiliwa na watu. Kwa hiyo, Serikali inaendelea kufanya tathmini ili kuona miradi mahususi ambayo itawekezwa katika eneo hili la KIA, nakushukuru sana.