Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 4 Planning and Investment Ofisi ya Rais: Mipango na Uwekezaji 46 2023-09-01

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:-

Je, ni miradi mingapi ya kimkakati imejengwa katika Wilaya ya Ileje?

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Mipango na Uwekezaji, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema Gerald Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati katika Halmashauri ya Wilaya ya Ileje ikiwemo ya uwekezaji wa madini, kilimo, biashara na uvuvi ambayo ina mchango mkubwa katika mapato ya Wilaya hiyo. Miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na:-

(i) Mradi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira.

(ii) Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Bwelui wa megawati 4.7 wenye thamani ya shilingi 19,675,520,200.

(iii) Mradi wa Ujenzi wa Soko la Kimataifa la Isongoole.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutekeleza Miradi mbalimbali ya Kimkakati kuilingana na fursa zinazopatikana nchini kwa lengo la kukuza uchumi, nakushukuru.