Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kufuatilia mila potofu za kuwekeza mke akiwa tumboni mwa mama hasa Manyara na Arusha?

Supplementary Question 1

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa kuozesha mtoto bila ridhaa yake ni unyanyasaji wa kijinsia; je, ni lini mwangozo huo utamalizika?

Swali la pili, je, kwa nini jambo hili lisiingizwe kwenye sheria? Ahsante sana.

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwongozo huu umeshakamilika na kinachofuata ni kuzindua. Kwa swali lake zuri la leo tutaenda kuzindulia Manyara hukohuko au Arusha na tutamualika na yeye awepo ili awe Balozi kabisa wa kubeba ujumbe huu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali pili kuhusu masuala ya sheria, ni kweli naona umuhimu huo, kwa sababu bado tunaendelea na mchakato wa maboresho ya Sheria ya Mtoto nimelipokea tutaliwasilisha kwenye Kamati waone itifaki ya kisheria kwa sasa kama inaweza kuingizwa au kunahitaji tafiti zaidi kisha tutawasilisha taarifa. Ahsante.(Makofi)

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kufuatilia mila potofu za kuwekeza mke akiwa tumboni mwa mama hasa Manyara na Arusha?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Je, Serikali ina mkakati gani wa kubaini mila zote nzuri ili kurithisha vijana wetu wa sasa waachane na mambo ya kigeni?

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Toufiq, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa nchini Tanzania tunazo mila nyingi sana nzuri ambazo kwa wakati wa sasa zingetusaidia kupambana na mabadiliko ya mmomonyoko wa maadili katika dunia nzima jinsi ambavyo inakumbwa. Hivyo basi, nimepokea hoja hii, tutakwenda kuunda kikosi kazi tukishirikiana na Wizara ya Utamaduni, Michezo na Sanaa pamoja na Wizara nyingine zote tuweze kuja na list ya hizo mila nzuri, kwa pamoja tuweze kuweka mkakati wa kuzielimisha, kuzithibitisha na kuziweka kwenye kumbukumbu sahihi za mila zetu ambazo tutakuwa tunazifanyia kazi Nchini.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kufuatilia mila potofu za kuwekeza mke akiwa tumboni mwa mama hasa Manyara na Arusha?

Supplementary Question 3

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Hivi karibuni kumeibuka utamaduni mzuri na mila nzuri sana ya kumtetea, kumlinda na kumjengea uwezo mtoto wa kike, lakini tunao utamaduni wetu ambao mtoto wa kiume ni baba au kiongozi wa familia: Je, Serikali ina mpango gani wa kumuimarisha na kumjengea uwezo mtoto wa kiume ili awe kiongozi mzuri wa familia? (Makofi)

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha, Mbunge, swali zuri kabisa, tuna utamaduni gani wa kumjengea uwezo mtoto wa kiume? Ni kweli kabisa tunatambua sasa hivi pia mtoto wa kiume tofauti na awali anakumbwa na changamoto nyingi sana zitokanazo na mmomonyoko wa maadili, anakosa malezi na makuzi bora, kiasi kwamba sasa hata akija kuwa baba atashindwa kuwa baba mzuri wa kupambana na changamoto za familia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili, Serikali inatekeleza mpango wa malezi na makuzi ya watoto kwenye umri wa awali ambapo hii inaenda sambamba na ujenzi wa vituo vya kulea watoto hawa kwenye ngazi ya jamii, na kule tunakuwa na watoto wa kiume na wa kike. Tuna mpango wa pili wa kuwawezesha na kuwaendeleza vijana balehe, kuanzia miaka 10 mpaka 19. Sasa hapa tutajikita tu kuongezea nguvu zaidi katika uwekezaji, pengine tuje na programu za kimkakati zinazojikita zaidi kwenye masuala ya watoto wa kiume.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zamani watoto walikuwa wanapelekwa jando, lakini sasa hivi tutakuwa tunapeleka jando la kisasa na miongozo yao mizuri mizuri inayosema maana ya kuwa baba pindi wanapokuwa vijana balehe wajue changamoto watakayokutana nayo huko kwenye ndoa kwamba ndoa siyo mchezo, lakini itawezekana kwa sababu tumewaandaa.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kufuatilia mila potofu za kuwekeza mke akiwa tumboni mwa mama hasa Manyara na Arusha?

Supplementary Question 4

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa mpango wa malezi na makuzi kwa mtoto ulishazinduliwa: Je, ni lini utekelezaji huu utaanza? Ahsante (Makofi)

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Suma, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango huu wa malezi na makuzi ya awali ya mtoto tulishauzindua tangu mwaka 2021, unakwenda mpaka 2026. Mojawapo ya afua zilizopo mle ni hizi za kujenga vituo hivi vya malezi na makuzi. Tayari vituo 200 vimeshajengwa kwenye maeneo mbalimbali ya jamii na sasa tunatafuta rasilimali na kuhamasisha jamii na wadau tuendelee kujenga kwenye maeneo ambayo yana hali mbaya zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mpango huu unatekelezwa na tayari kuna watoto wapo humo wanapata hizi huduma na jamii imethibitisha kwamba kweli sasa hivi wazazi wanapata amani ya kwenda kutafuta maendeleo huku watoto wao wakiwa salama. Tutaongeza kasi hii na tutaleta taarifa kupitia Kamati zetu tunavyoendelea. (Makofi)