Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kufufua Kiwanda cha General Tyre na shamba la mpira Kata ya Mwaya-Kilombero?

Supplementary Question 1

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa kufanya ziara jimboni karibu mara mbili, ametembelea kiwanda cha Kilombero Sugar na Mang’ula Machine Tools pamoja na shamba hili la rubber.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza. Shamba hili ambalo lina ukubwa wa karibu hekari 1,678; sasa hivi kuna watu wachache kwa manufaa yao wanalikodisha kwa wananchi: Kwanini Serikali kupitia Serikali ya Kata isitoe uwazi eneo la shamba ambalo halijapandwa rubber, lilimwe na wananchi mpunga au miwa kwa uwazi tofauti na ilivyo sasa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Ili kuweka ulinzi wa shamba hilo, tuliwasilisha ombi letu kwa Mheshimiwa Waziri kutoa sehemu ya shamba kwa maslahi ya maendeleo ya wananchi kwa ujenzi wa kituo cha polisi, high school na kituo cha afya: Je, ombi letu limefikia wapi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ni kweli kulikuwa na changamoto hizi za uvamizi katika shamba hili la mpira. Namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa kuleta taarifa hii ambayo kimsingi hairuhusiwi watu kufanya shughuli nyingine nje ya shughuli tarajiwa katika shamba hili la mpira.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama kuna uvamizi huo, naomba niielekeze NDC waweze kufuatilia ili kama kweli kuna haja ya wananchi kutumia maeneo ambayo hayajaanza kuendelezwa kwa kupanda miti ya mpira, basi tuone namna ya utaratibu mzuri kama ambavyo ameshauri Mheshimiwa Mbunge kupitia viongozi wa Kata na eneo husika ili wananchi wa pale waweze kufaidika na kutumia eneo hilo ambalo ni la Serikali, kwa utaratibu kamili. Kimsingi, eneo hili ni la kuzalisha miti kwa ajili ya mpira.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili kama alivyosema Mbunge, Mheshimiwa Waziri amepitia katika shamba hili, tunaendelea kujadiliana tuone namna gani tunaweza kuwezesha huduma hizi za kijamii kwa maana ya shule, vituo vya afya au kituo cha polisi, tuone kama vinaweza kujengwa katika eneo hili la shamba ambapo kimsingi ni kwa ajili ya uzalishaji wa mpira, nakushukuru.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kufufua Kiwanda cha General Tyre na shamba la mpira Kata ya Mwaya-Kilombero?

Supplementary Question 2

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Je, ni nini mpango wa Serikali katika kufufua viwanda vilivyotelekezwa kwa muda mrefu kikiwemo kiwanda cha kuchambua pamba cha Nyambiti kinachopatikana katika Kijiji cha Mwabilanda katika Jimbo la Sumve?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Ni kweli moja ya maeneo ambayo Serikali tunaweka mkazo sasa ni kuona tunafufua viwanda ambavyo vilikuwa vimebinafsishwa, na baadhi ya maeneo au viwanda hivyo wale wawekezaji tuliowabinafsia hawajavifufua au kuviendeleza au wanafanya tofauti na mkataba tuliowapa. Pamoja na viwanda vingine, hiki pia kipo kwenye mpango huo ambapo tunaendelea kutafuta wawekezaji au kuhakikisha wale ambao tumewakabidhi kwa sasa, waweze kuviendeleza kulingana na mikataba ambayo tulikuwa tumeingia nao, nakushukuru.