Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 2 Industries and Trade Wizara ya Viwanda na Biashara 40 2023-08-30

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kufufua Kiwanda cha General Tyre na shamba la mpira Kata ya Mwaya-Kilombero?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abubakari Damian Asenga, Mbunge wa Kilombero, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Kiwanda cha Matairi Arusha, uko kwenye hatua ya kukamilisha taratibu za kuutangaza ifikapo mwezi Oktoba, 2023 ili kuweza kumpata mwekezaji mahiri mwenye mtaji na teknolojia ya kisasa inayohitajika. Mradi huu unatarajiwa kutangazwa ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa mashamba ya mpira likiwemo shamba la Kilombero, Serikali kupitia Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) imeendelea kuboresha uzalishaji wa mpira kwa kupanda miche mipya, kujenga miundombinu, kununua mashine za kugemea utomvu, uchakataji na vitendea kazi vingine ili kuongeza upatikanaji wa utomvu na mpira mkavu wenye viwango bora, nakushukuru.