Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aleksia Asia Kamguna

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuzuia wafugaji kuchunga mifugo katika Hifadhi ya Julius Nyerere?

Supplementary Question 1

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia kwenye mbuga zetu kuna Askari pamoja na Maafisa wengine ambao wanazilinda hizo mbuga. Ukienda kule kwenye mbuga utakuta kuna vibanda vya wafugaji wanaishi huko pamoja na rundo la mifugo wakati Serikali wanasema kwamba wameweka zuio. Je, hao wafugaji walioko kule na hivyo vibanda hawa Askari hawawaoni? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili. Inasemekana kuna baadhi ya Maafisa Wanyamapori ambao siyo waaminifu, wanashirikiana na wale watu wenye mifungo kuwaingiza katika hifadhi zetu. Je, Serikali inasemaje katika hili? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Aleksia Kamguna, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba hawa Askari wanakuwepo katika maendeo ya hifadhi, changamoto ambayo tunakutana nayo hasa kwenye mapori ambayo yameungana na mapori ya Halmashauri na mengine ni mapori ya Vijiji. Kwa mfano, kama Hifadhi ya Nyerere, tuna Hifadhi ya Selous lakini kuna mapori ambayo yameungana na Hifadhi ya Nyerere. Kwa hiyo, utakuta kwamba kwenye Pori la Selous Askari wanafanya operesheni, pale ambapo kunakuwa na mifugo, inakamatwa na inachukuliwa hatua lakini wale wamiliki wahiyo mifugo wanaenda wana-pause kwenye yale mapori ya Halmashauri pamoja na Vijiji ambapo sasa kule askari wetu hawafiki katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, changamoto hiyo imekuwa kubwa kwa sababu hii mifungo ipo na inakuwa kando kando tu inakuwa imeegeshwa pale ambapo Askari wetu wanapoondoka tu tayari mifugo inaendelea kuingia hifadhini, lakini kulingana na sheria zetu, nadhani wanafahamu wafugaji namna ambavyo tunasimamia kanuni, taratibu na namna ambavyo tunaendelea kuzishughulikia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye hili suala la Askari kushirikiana na Wafugaji. Ni kweli tuna sheria kali sana na pale inapogundulika kwamba Askari anashirikiana na kukiuka kanuni na taratibu zilizopo, tunamchukulia hatua mara moja na wengine wanafukuzwa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii sheria tunatumia Sheria ya Jeshi ambayo tayari sisi tumeshaanza kuingia katika utaratibu huu na wengi wameshachukuliwa hatua. Kwa hiyo, ikithibitika kwamba kuna Askari amefanya hivi basi tupate taarifa mara moja na tuweze kuchukua hatua. (Makofi)

Name

Riziki Saidi Lulida

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuzuia wafugaji kuchunga mifugo katika Hifadhi ya Julius Nyerere?

Supplementary Question 2

MHE. RIZIKI S. LULIDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Lindi sasa hivi, eneo la Selous pamoja na Mbuga ya Tendeguru kuvamiwa na wafugaji. Mheshimiwa Naibu Waziri ni shahidi, alikwenda akawakuta wafugaji wako ndani ya mbuga, wakichoma mikaa katika Misitu ya Tendeguru na kumaliza Miti ya Mipingo lakini kusababisha sasa hivi taharuki, Wafugaji kutoka katika misitu, kwenda kuvamia mashamba ya watu. Sasa hivi Mkoa wa Lindi tuko katika taharuki kubwa ya mapigano ya wafugaji na wananchi.

Je, Mheshimiwa Waziri aliyepo pale anatoa tamko gani leo hapa kwa vile aliyaona haya lakini utekelezaji wake haukukamilika mpaka hivi sasa?

Mheshimiwa Naibu Spika, nawasilisha swali langu. Ahsante.(Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Sisi kama Serikali tumeshajipanga, kwa maana ya Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, tukae pamoja kwa sababu suala hili ni suala la wananchi wetu na hao wananchi nao wanayo haki ya kuishi kama Watanzania. Tunachokifanya sasa hivi tunasimamia sheria upande mmoja lakini upande wa pili wanaegesha tu wanasubiria kuingia tena.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo sisi kama Serikali tukae pamoja, tuone namna iliyo bora ya kuwahudumia hawa wafugaji ili changamoto hii sasa isiendelee kujitokeza. Kwa sababu sasa hivi sisi tumepewa dhamana.