Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 2 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 35 2023-08-30

Name

Aleksia Asia Kamguna

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuzuia wafugaji kuchunga mifugo katika Hifadhi ya Julius Nyerere?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aleksia Asia Kamguna, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ya Uhifadhi Wanyamapori Sura Namba 283 iliyorejewa mwaka 2022, Sheria ya Hifadhi za Taifa Sura 282 na Sheria ya Misitu ya mwaka 2002, zimeweka zuio la kuingiza mifugo ndani ya maeneo ya hifadhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto ya uingizaji wa mifugo katika maeneo yaliyohifadhiwa ikiwemo Hifadhi ya Taifa Nyerere ni ya muda mrefu. Wizara inakabiliana na changamoto hii kwa kuimarisha doria katika maeneo ya hifadhi na kuwachukulia hatua wanaoingiza mifugo hifadhini kwa mujibu wa Sheria na Kanuni zilizopo. Aidha, Wizara inaendelea kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kukabiliana na changamoto hiyo.