Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha inapata data za bidhaa zote za kilimo zinazosafirishwa nje ya nchi?

Supplementary Question 1

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza. Tumekuwa tukiona wanunuzi kutoka nje ya nchi wakija kununua mazao moja kwa moja wakiwa na magari yao ambayo yana namba za nje ya nchi; na tumekuwa tukiona wananchi wanauziwa kwa bei za chini sana, hasa mazao ya parachichi na mazao mengine kwa sababu hawana mtu anayewasimamia vizuri. Je, mnunuzi anapoenda kununua mazao hayo moja kwa moja kwa sasa hizo data wanazichukuwaje?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa Serikali imekiri kabisa inaendelea kuboresha huo mfumo wa ATMIS na TANCIS ni lini maboresho hayo yatakwenda kukamilika kwa sababu tumeona kwamba, bidhaa zinaenda nje ya nchi na tumekuwa hatujui mchango kamili wa kilimo kwa fedha za kigeni.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la kwanza, ni kweli kumekuwepo na baadhi ya wanunuzi ambao wanakwenda moja kwa moja mashambani, ndiyo maana Waheshimiwa Wabunge mtakumbuka tulileta utaratibu wa namna ya ununuzi wa mazao ili wale wote ambao wanataka kununua mazao nchini Tanzania wafuate utaratibu na mwisho wa siku sisi kama Serikali tupate takwimu sahihi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali ni nini katika hili. Jambo la kwanza, katika eneo la mazao ya nafaka, hivi sasa tunataka kuboresha, kutengeneza masoko ili bidhaa zote zipelekwe katika masoko na wanunuzi wakanunue katika masoko yanayotambuliwa ili kupata takwimu sahihi.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, kwenye mazao ya mbogamboga na matunda, hivi sasa tunajenga common use facilities tatu za kuanzia katika eneo la Nyororo, Hai na Kurasini, ambapo kwa mfano parachichi yote itakusanywa, tutafanya grading, sorting na packaging ambayo itatupa pia uhakika wa kujua ni parachichi kiasi gani imekusanywa na kupelekwa nje ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo, swali lako la pili kuhusu mifumo hii, kama mnavyofahamu Waheshimiwa Wabunge mifumo hii siyo jambo la siku moja. Tunaendelea kuiboresha kutokana na maendeleo ya teknolojia vilevile na ukuaji wa soko.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano kwa hivi sasa, tunao mfumo wetu ukiacha hii mifumo mingine wa kutumia mamlaka ya afya, mimea na viuatilifu, ambao wao wanawajibu wa kutoa phytosanitary kwa bidhaa zozote ambazo zinatoka nje ya nchi, cheti cha usafi wa mazao pia na wenyewe ni mfumo ambao tumewaunganisha kutupa takwimu sahihi. Kwa hiyo, hakuna mtu aliye na uwezo wa kusafirisha mazao nje ya nchi kama hajapata export permit na phytosanitary certificate ambayo pia inatupa nafasi ya kuweza kujua ni mazao kiasi gani yamesafirishwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tutaendelea kuboresha mfumo huu ili tupate takwimu sahihi ya mazao yetu.