Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Banio la Maji, Kata ya Endagau, Wilaya ya Hanang?

Supplementary Question 1

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nichukue nafasi hii mimi pamoja na wananchi wa Kata ya Endagaw na wananchi wa Wilaya ya Hanang, kuiomba Serikali kuhakikisha kwamba ujenzi huo wa mifereji unafanyika sasa na sio kipindi cha masika kwa sababu sisi tunajua uhalisia wa jiografia tunapotoka.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; kwa kuwa wananchi wa Wilaya ya Hanang ni wananchi ambao wanalima sana. Je, Serikali haioni haja sasa ya kuendelea kuongeza mabwawa ili wananchi wa Wilaya ya Hanang waweze kulima kilimo cha uhakika na chenye tija? Ahsante sana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, baada ya kumwondoa mkandarasi aliyeshindwa kufanya kazi yake vizuri, hivi sasa tunahakikisha kwamba mkandarasi ambaye tutamtangaza aifanye kazi hii kwa haraka na kuwahi msimu huo ambao umekuwa na athari kubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Waziri, la pili, ni kweli Wilaya ya Hanang ina wakulima wengi. Katika mpango wa Serikali, mwaka huu wa fedha tutakwenda kuchimba bwawa eneo la Laganga ambapo zaidi ya hekta 600 za umwagiliaji zitapatikana na wakulima wa eneo la Hanang watapata maeneo ya kilimo chao cha umwagiliaji. (Makofi)

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Banio la Maji, Kata ya Endagau, Wilaya ya Hanang?

Supplementary Question 2

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Serikali kupitia Wizara ya Kilimo mradi wake wa DASP walifika Ngara mwaka 2015, wakaanza kujenga Skimu ya Umwagiliaji ya Vigombo, wakaitelekeza ikiwa imefika katikati kwa zaidi ya miaka nane iliyopita. Je, ni lini Wizara ya Kilimo itafika Ngara na kuja kukamilisha Mradi wa Skimu ya Umwagiliaji ya Vigombo? Ahsante sana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha miradi yote ya umwagiliaji inakamilika na ndiyo maana tumewekeza fedha nyingi kwa ajili ya ukarabati na kuipitia. Nichukue fursa hii kumuahidi Mheshimiwa Mbunge ya kwamba nitampa maelekezo Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji aelekee katika eneo la Rulenge pale Vigombo ili aangalie mradi huu na tuone namna ya kuweza kuwakwamua wananchi ili wafanye kilimo cha umwagiliaji.

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Banio la Maji, Kata ya Endagau, Wilaya ya Hanang?

Supplementary Question 3

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itakamilisha kujenga miundombinu ya umwagiliaji, hasa kusakafia mifereji mikuu katika Skimu ya Mangisa na Diri iliyoko Wilayani Mbulu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, tumeendelea kuipitia miradi yote ya skimu za umwagiliaji ambayo ilikuwa ina changamoto na tumetenga fedha za mwaka huu na mwaka wa fedha ujao. Hivyo, nitakaa na Mheshimiwa Mbunge kuangalia katika mwaka huu kama haijawekwa kwenye bajeti hii, basi tuitengee bajeti inayokuja ilimradi tu wakulima waweze kupata fursa ya kufanya kilimo cha umwagiliaji.