Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 2 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 31 2023-08-30

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Banio la Maji, Kata ya Endagau, Wilaya ya Hanang?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asia Abdukarimu Halamga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji Endagaw iliyopo katika Mkoa wa Manyara, Wilaya ya Hanang ulianza mwaka wa fedha 2021/2022. Hadi sasa Serikali imeshakamilisha ujenzi wa baadhi ya maeneo ikiwemo ujenzi wa ukuta wa bwawa wenye takribani mita 270 pamoja na punguza maji (Spillway) na baadhi ya maumbo ya mradi huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imepanga kukamilisha ujenzi wa kazi zote zilizobaki, hii ni baada ya kukamilisha mapitio ya usanifu wa mradi huu, ikiwemo mfereji wa Onjae pamoja na maumbo yake.