Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali italipa fidia eneo la Nanganga ambako ujenzi wa barabara iendayo Ruangwa unaendelea?

Supplementary Question 1

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza sikubaliani na majibu yaliyotolewa na Serikali na swali hili limerudi kwa mara ya pili baada ya maelekezo ya Mheshimiwa Spika wakati fulani hapo nyuma kwa sababu zifuatazo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo hili tunalolizungumzia barabara ilihama kwenye original plan na barabara hii imewafuata wananchi. Kwa sababu hiyo haina qualification ya mita 22 wala mita hizo zinazotajwa 22.5 wala nyongeza ya mita 7.5. Mheshimiwa Waziri Mbarawa alifika kwenye hiki kijiji tarehe 22 mwezi wa kwanza, mwaka 2022 eneo ambalo Misikiti, Kanisa pamoja na Nyumba za Serikali zilivunjwa. Swali langu la msingi ni lini Serikali itakwenda kulipa fidia kwa sababu wenyewe walifuatwa na barabara na si wao waliifuata barabara? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi; kwamba kama barabara imemfuata mwananchi ama imehama na kwenda sehemu ambayo haikuwepo maana yake hawa watu wanastahili fidia; na kama suala alilolielezea Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara imehama kabisa. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wananchi hawa watakuwa wanastahili fidia. Kwa hiyo, kwa sababu swali lake ni specific na eneo linalohusika, naomba baada ya hapa tuweze kukutana naye ili tuweze kuangalia. Kama barabara iliwafuata hawa wananchi kama alivyosema basi wananchi hao wana haki ya kulipwa fidia. Ahsante.

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali italipa fidia eneo la Nanganga ambako ujenzi wa barabara iendayo Ruangwa unaendelea?

Supplementary Question 2

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza;

Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi waliopisha Barabara ya Mianzini – Sambasha - Kimyaki hadi Ngaramtoni?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama Ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli barabara hii ni mpya na imefunguliwa. Tayari tulishandaa taratibu za kuwalipa wananchi ambao tumeifungua ile barabara, na barabara iliyoanza ni mpya wananchi hao watalipwa mara baada ya kukamilisha taratibu zote za fidia, ahsante. (Makofi)

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali italipa fidia eneo la Nanganga ambako ujenzi wa barabara iendayo Ruangwa unaendelea?

Supplementary Question 3

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa tangu tathmini ya malipo ya fidia kwa wananchi wa Nanganga yamefanyika muda mrefu umepita.

Je, Serikali iko tayari kuongeza kiwango cha fidia kwa wananchi wale kwa sababu walisimama kabisa katika maendeleo yao? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni utaratibu wa Serikali kwamba kama fidia imefanyiwa tathmini ikapita miezi sita ni lazima turudi kuhuisha tena ile tathmini ili kupata thamani ya wakati huo. Kwa hiyo itafanyiwa tathmini mpya kama imepita miezi sita na watalipwa sasa fidia ya wakati huu, ahsante. (Makofi)

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali italipa fidia eneo la Nanganga ambako ujenzi wa barabara iendayo Ruangwa unaendelea?

Supplementary Question 4

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Napenda kuuliza barabara ya Bypass ya Uyole – Songwe, ni lini wananchi watalipwa fidia waliopisha hiyo barabara ya bypass?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE.ENG GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, barabara inayotajwa ndiyo kwanza wakandarasi wameshakabidhiwa, na ipo kwenye huu mpamgo wa EPC+F. Jana nilijibu kwamba moja ya vitu ambavyo sasa hivi vinafanyika ni kupitia upya na kufanya tathmini ya malipo yatakayofanyika kwa ajili ya wale wananchi ambao watapisha, ikiwa ni pamoja na wananchi wa hiyo Barabara ya Uyole – Songwe Bypass. Ahsante.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali italipa fidia eneo la Nanganga ambako ujenzi wa barabara iendayo Ruangwa unaendelea?

Supplementary Question 5

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Barabara ya Makofia- Mlandizi – Mzenga mpaka Vikumbulu miaka mitatu iliyopita walifanyiwa tathmini ya kilomita 30 na miezi miwili iliyopita wamerudi kubadilisha kurudi kwenye mita 22.5;

Je, ni lini wananchi wale watalipwa fidia pamoja na mabadilko hayo? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge, tayari tumekwenda kwa ajili ya kufanya tathmini kwa watu ambao wapo ndani ya mita 22.5. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba maandalizi yanafanyika ndiyo maana tumekwenda sasa hivi ili waweze kulipwa fidia. Ahsante.