Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 2 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 25 2023-08-30

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali italipa fidia eneo la Nanganga ambako ujenzi wa barabara iendayo Ruangwa unaendelea?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecil David Mwambe, Mbunge wa Ndanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Barabara Na. 13 ya Mwaka 2007 na Kanuni zake za Mwaka 2009 wananchi ambao mali zao zipo ndani ya mita 22.5 hawatastahili kulipwa fidia kwani wamo ndani ya eneo la hifadhi ya barabara. Kwa upande wa wananchi ambao wamo ndani ya nyongeza za mita 7.5 kwa nchi nzima Serikali inafanya kazi na kuandaa mapendekezo ambayo yatabainisha maeneo gani wananchi wataruhusiwa kuyaendeleza na yapi Serikali itayachukua na kuyalipa fidia. Ahsante.