Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kudhibiti vyombo vya baharini vinavyozidisha mizigo na abiria?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ambayo ameegemea zaidi kwenye mtazamo wa Sheria badala ya hali halisi ilivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Je, ni lini mmechukua hatua kwa meli zilizozidisha abiria na kusababisha vifo vingi zaidi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania inavyombo vingapi? Vinavyotoa huduma za abiria na mizigo baharini na maziwa makuu? Ahsante. (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, Mwantumu Dau Haji, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kuna baadhi ya vyombo huwa vinakiuka sheria kwa kuzidisha uzito wa abiria na mizigo. Kupitia TASAC tunatoa elimu kwa wamiliki wa vyombo hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spaka, pili; sheria inatutaka kwa yeyote atakayezidisha uzito kulipa faini na kabla meli haijaondoka kuna Maafisa ambao wanahakikisha mstari wa ujazo haujazidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, faini hizo zinatofautiana kulingana na urefu wa chombo na chombo. Chombo chenye urefu wa mita zaidi ya 24 wanalipa faini ya shilingi laki nne na chombo chenye urefu chini ya mita 24 wanalipa faini ya shilingi laki mbili lakini ikithibitika pia huyo mmiliki ameshindwa kulipa faini hiyo anapelekwa Mahakamani.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ameuliza idadi ya vyombo tulivyonavyo hapa nchini. Kwa Sensa ambayo ilifanywa na TASAC mwaka 2021 kwa kushirikiana na Ofisi ya Mtakwimu wa Taifa (NBS) inaonesha vyombo vyote tulivyonavyo hapa nchini kwa ukanda wa bahari, maziwa makuu yote, mito na maziwa madogo ni 52,189; hii ndiyo takwimu iliyofanyika mwaka 2021. Na kati ya vyombo hivyo asilimia 53.6 vipo Ziwa Victoria, asilimia 13.4 vipo Bahari ya Hindi, asilimia 10.2 vipo Ziwa Tanganyika, asilimia 7.6 vipo Ziwa Nyasa na asilimia 15.2 vipo maeneo ya Maziwa Madogo pamoja na Mito. Ahsante.