Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 2 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 24 2023-08-30

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kudhibiti vyombo vya baharini vinavyozidisha mizigo na abiria?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantum Dau Haji, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vyombo vikubwa ikiwa ni vyombo vyenye urefu zaidi ya mita ishirini na nne. Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania TASAC linajukumu kisheria kufanya ukaguzi wa michoro ya meli kabla ya hatua ya ujenzi kuhakikisha mstari wa ujazo (load line) umewekwa kwenye kina sahihi cha meli, kisha Msajili wa meli anathibitisha michoro hiyo na kutoa ruhusa ya ujenzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, TASAC kufanya ukaguzi kipindi cha ujenzi wa meli. TASAC hufanya Ukaguzi kuhakikisha Meli inapakia mizigo bila kupitiliza mstari wa ujazo uliothibitishwa na Msajili, na endapo itabainika kuwa meli imezidisha ujazo wa abiria, mizigo au vyote kwa pamoja itakuwa imetenda kosa kisheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, meli hiyo itapaswa kuzuiliwa bandarini na Mamlaka ya Bandari Tanzania itajulishwa ili kusitisha kutoa kibali kwa meli hiyo hapo bandarini. Kwa hatua zaidi, TASAC humtoza mmiliki au nahodha wa meli faini na kisha kusimamia upunguzwaji wa abiria, mizigo na vyote kwa pamoja kisha kuruhusu meli hiyo pindi Mkaguzi atakapojiridhisha kuwa Meli ipo salama kwa kuanza safari.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa vyombo vidogo vyenye urefu chini ya mita ishirini na nne, TASAC inajukumu kisheria kufanya ukaguzi wa vyombo vidogo na kutoa leseni ya uendeshaji inavyotaka ujazo wa abiria au mizigo unaostahili kuzingatiwa katika uendeshaji wa chombo.

Mheshimiwa Naibu Spika, endapo itabainika kuwa chombo kimezidisha ujazo wa abiria au mizigo, nahodha atakuwa ametenda kosa kisheria na chombo hicho kitazuiliwa bandarini au mwaloni ili kulipa faini na TASAC kusimamia upunguzwaji wa abiria au mizigo kabla ya kuruhusu chombo kuendelea na safari, ahsante.