Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Songambele ili kupunguza msongamano kwenye Kituo cha Afya Nkwenda Wilayani Kyerwa?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, swali langu la kwanza, kwenye Wilaya ya Kyerwa tunayo maboma ambayo yanazidi ya miaka 10 mpaka 15. Kwa mfano Kata ya Kimuli kuna boma ambalo linazaidi ya miaka 15 halijakamilishwa na ni nguvu ya wananchi. Kata ya Kikukuru kuna Zahanati ya Omkutembe na yenyewe haijakamilika zaidi ya miaka 10. Je, ni lini Serikali itakamilisha maboma haya ili wananchi waweze kupata huduma? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bilakwate, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kutoa fedha kwa ajili ya ukamililishaji wa maboma ambayo yameanza kujengwa kwa nguvu za wananchi nchini kote na mpaka mwezi Juni mwaka huu jumla maboma elfu moja na sitini na sita Serikali ilikuwa imepeleka fedha yamekamilishwa ujenzi wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, zoezi hili linaendelea kwa awamu. Kwa hiyo, ni mhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba maboma haya ya zahanati yenye umri mrefu wa miaka 10 na zaidi yatapewa kipaumbele kwenye bajeti za Serikali. Pia naelekeza kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, kwamba Halmashauri hii ya kyerwa watenge pia mapato ya ndani kuhakikisha wanakamilisha majengo haya kwa huduma za wananchi, ahsante. (Makofi)

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Songambele ili kupunguza msongamano kwenye Kituo cha Afya Nkwenda Wilayani Kyerwa?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kituo cha Afya Kiloleni Wilaya ya Busega hakina wodi za kulaza wagonjwa, wodi ya wanaume, wanawake na watoto. Je, ni lini Serikali itajenga wodi hizo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu, Mbunge wa viti maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kituo cha Afya cha Kiloleni katika Halmashauri ya Busega hakina wodi za kulaza wagonjwa. Niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge, kwamba vituo hivi vya afya vinajengwa kwa awamu. Tunaanza na awamu ya kwanza ya majengo ya OPD, Maabara lakini pia majengo ya mama na mtoto na majengo ya upasuaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua zinazofuata ni kukamilisha kujenga mawodi na miundombinu mingine. Kwa hiyo, ni mhakikishie Mheshimiwa Mbunge, muda huo utakapofika tutahakikisha pia tunatafuta fedha kwa ajili ya kituo hiki cha afya cha Kiloleni, ahsante. (Makofi)

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Songambele ili kupunguza msongamano kwenye Kituo cha Afya Nkwenda Wilayani Kyerwa?

Supplementary Question 3

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Halmashauri ya Busekelo wananchi wamejenga maboma kwa ajili ya vituo vya afya, maboma manne. Ikiwa ni Kata ya Lufilyo, Kisegese, Mpombo na Kambasegela. Je, ni lini Serikali itaunga juhudi za wananchi hao kukamilisha maboma hayo ya vituo vya afya? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Suma Fyandomo, Mbunge wa viti maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niwapongeze wananchi wa Jimbo la Busekelo kwa kutoa nguvu zao kuanzisha ujenzi wa maboma ya vituo vya afya, lakini niwahakikishie tu kwamba, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha vituo vya afya kwenye kata za kimkakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunakwenda kufanya tathimini kuona kati ya hayo maboma lipi ni lakimkakati ili Serikali itafute fedha kwa ajili ya kuwaunga mkono kukamilisha maboma hayo, ahsante. (Makofi)

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Songambele ili kupunguza msongamano kwenye Kituo cha Afya Nkwenda Wilayani Kyerwa?

Supplementary Question 4

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Serikali ilitoa fedha kwa ajili ya kujenga Kituo cha Afya cha Kabwe, lakini mpaka leo kile kituo hakijakamilika kwa sababu fedha hazitoshi. Ni mkakati upi wa Serikali wa kumalizia kituo kile cha afya ili wananchi wa Kabwe wapate huduma pamoja na kata ya jirani ya Korongwe? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kituo cha afya cha Kabwe kilipelekewa fedha na Serikali kwa ajili ya ujenzi na kwa taarifa kwamba hakijakamilika tutakwenda kwanza kujifunza kwa nini fedha iliyopelekwa haijakamilisha majengo. Kama kuna matumizi mabaya ya fedha ya Serikali wanaohusika watakaothibitika tutachukua hatua za kisheria na za kinidhamu. Lakini pia tutatafuta pia fedha kuhakikisha kwamba kituo kinakamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi.