Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tamima Haji Abass

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TAMINA HAJI ABASS aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kukarabati nyumba za makazi ya Askari Polisi Kaskazini Unguja?

Supplementary Question 1

MHE. TAMINA HAJI ABASS: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya matumaini ya Mheshimiwa Waziri, naomba kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa vile fedha hizo zitatengwa kwenye bajeti ya mwaka ujao; je, itawasaidiaje askari wanawake ambao wanaishi mbali na vituo vyao vya kazi? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo imeelezwa, nyumba hizi 14 zitakapokarabatiwa, mgao wa nyumba hizo kwa Askari wetu uzingatie uwiano wa jinsia ili Askari wa kike ambao Mheshimiwa ana mashaka kwamba wanakosa nyumba za kuishi waweze kupata nyumba, nashukuru.

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. TAMINA HAJI ABASS aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kukarabati nyumba za makazi ya Askari Polisi Kaskazini Unguja?

Supplementary Question 2

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwanza nachukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Naibu Waziri baada ya kukubali ombi letu la wananchi wa Jimbo la Chumbuni kutupa ruhusa ya kujenga kituo chetu kikubwa cha Polisi ambacho tunaendelea nacho hivi sasa. Kama swali la msingi lilivyoulizwa kuhusu matatizo ya makazi, nasi tunatarajia kuwa na kituo kikubwa cha Class C; je, anatuahidi nini katika tatizo hili la makazi kwa sababu tunajenga kituo kikubwa? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, tunaweka kipaumbele na kila tunapojenga kituo kikubwa cha polisi, tunazingatia pia makazi ya askari na viongozi wa Jeshi la Polisi. Ushauri wangu kwa Mheshimiwa Mbunge, ni kuhakikisha linapatikana eneo ili mpango wa ujenzi uende sambamba na kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za vijana wetu, nashukuru sana. (Makofi)