Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 17 2023-08-29

Name

Tamima Haji Abass

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TAMINA HAJI ABASS aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kukarabati nyumba za makazi ya Askari Polisi Kaskazini Unguja?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tamina Haji Abass, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tathmini kwa ajili ya ukarabati wa nyumba zote 14 za makazi ya askari polisi katika Mkoa wa Kaskazini Unguja, imefanyika na kiasi cha shilingi 447,065,000 zinahitajika. Fedha hizo zinatarajiwa kutengwa kwenye Bajeti ya Serikali ya 2024/2025, ahsante.