Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohammed Said Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliauliza: - Je, hesabu zinazowasilishwa na CAG kila mwaka ni za mashaka au uhakika?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED SAID ISSA: Mheshimiwa Spika, ahsante, nina maswali mawili ya nyongeza.

Je, wale waliokutwa na ubadhirifu wamechukuliwa hatua gani?

Swali la pili, je, Serikali itakuwa tayari kuweka utaratibu wa kuutangazia umma wale waliochukuliwa hatua pamoja na hatua zilizochukuliwa ili kuwafanya Watanzania waweze kuiamini Taasisi hii ya CAG? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, tunalipokea wazo la Mheshimiwa Mbunge na hivi ndivyo ambavyo tumekuwa tukifanya kwamba wale ambao wanabainika kuwa na makosa wanachukuliwa hatua. Mpaka sasa kuna hatua mbalimbali ambazo zinaendelea baada ya taarifa ya CAG kukamilika. Baada ya majibu ya Serikali kutolewa yale maeneo yanayoonekana kuwa na hatia ndani yake yanakwenda kwenye uchunguzi na sasa hivi tuna majalada ambayo yako ngazi ya uchunguzi na tuna yale ambayo yalishafika ngazi za kimahakama. Pia kuna maeneo ambayo kesi zilishahukumiwa ambazo zinahusisha upotevu ambao taarifa zake zimepatikana kupitia taarifa ya CAG.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kutangaza tumepokea hilo, tutaboresha vitengo vya mawasiliano ili vianze kutoa matamko kwenye maeneo ambayo hatua zimechukuliwa pale ambapo kulikuwa na ubadhirifu umebainika kupitia taarifa ya CAG.