Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 1 Finance Wizara ya Fedha 15 2023-08-29

Name

Mohammed Said Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliauliza: -

Je, hesabu zinazowasilishwa na CAG kila mwaka ni za mashaka au uhakika?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohammed Said Issa, Mbunge wa Konde, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hesabu zinazowasilishwa na Maafisa Masuuli kwa CAG kila mwaka ni za uhakika kwa kuwa zinaandaliwa kwa kuzingatia matakwa ya kifungu cha 30(2) cha Sheria ya Fedha za Umma, Sura 348, Viwango vya Kimataifa vya Uhasibu katika Sekta ya Umma (IPSAS), miongozo mbalimbali inayotolewa na Wizara ya Fedha na mifumo madhubuti ya kielektroniki ya usimamizi wa fedha ikijumuisha Mfumo wa Uhasibu Serikalini (MUSE).

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita (2019/2020 – 2021/2022), taarifa ya CAG imeonesha ongezeko la hati zinazoridhisha kutoka asilimia 92 mpaka 96 kwa Serikali Kuu, asilimia 70 mpaka 94 kwa Serikali za Mitaa na kupungua kutoka asilimia 97 mpaka 98 kwa Mashirika na Taasisi nyingine za Umma.