Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawasaidia wanawake na vijana wa Kata za Mitesa na Nanjota wanaojihusisha na uchimbaji madini Lulindi?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, sababu kubwa ya kutokushiriki kikamilifu kwa vijana na wanawake katika shughuli hii ya madini ni mikopo kwa maana ya capital.

Je, Serikali haioni sababu ya kuwapa vijana mitaji ili kusudi washiriki kikamilifu katika sekta hii? (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, napenda kumjibu Mheshimiwa Mchungahela mtetezi makini wa watu Jimbo la Lulindi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli changamoto kubwa ya vijana, wanawake na wachimbaji mbalimbali ni ukosefu wa mitaji. Katika kutanzua changamoto hii Wizara ya Madini kupitia Shirika lake la Taifa la Madini (STAMICO) wamewaweka wakfu walezi wakuu wa wachimbaji wadogo na hatua za awali za kuwasaidia zimehusisha kutoa elimu ili wafahamu namna ya kufanya uchimbaji wa tija, Sheria ya Madini, pia kuingia katika makubaliano na taasisi za kifedha hapa nchini zikiwemo Benki za NMB, CRDB na Azania ili waweze kuwakopesha wale ambao wamekidhi vigezo.

Mheshimiwa Spika, ili waweze kusaidiwa, wananchi wa Jimbo lake na Watanzania wote ambao wamepata hamasa ya kujihusisha na biashara ya madini ni vizuri waunde vikundi ili kuwa rahisi kuwafikia na kuwasaidia kupitia vikundi na wajiunge na Chama cha Wachimbaji wadogo wa Madini Tanzania ambao sasa hivi wapo kwenye mchakato wa kuanzisha benki yao ili waweze kupata mitaji na waweze kuchimba kwa wakati kwa tija zaidi na wa ufanisi.