Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU sliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo la uhaba wa Hosteli kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu wanaosoma katika Vyuo vya Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 1

MHE. NORAH W. MZERU: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi, ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina swali moja la nyongeza.

Je, Serikali itawasaidiaje wamiliki wa nyumba za kulala wenye nia ya kubadilisha matumizi na kuzifanya hostel hasa katika suala la tozo za Serikali?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mzeru kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, suala la kubadilisha matumizi ya nyumba pamoja na ardhi yapo kwa mujibu wa sheria, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba taratibu hizo wamiliki wa nyumba pamoja na ardhi wanapaswa kuzifuata, lakini kwa vile wanafanya biashara ni lazima zile taratibu zingine za tozo pamoja na kodi ya Serikali ni lazima zilipwe. Kwa hiyo, ni muhimu kwa wale wamiliki wanapobadilisha matumizi kwenda kwenye mamlaka husika kutoa taarifa ya kubadilisha zile leseni zao za biashara ili waweze kupata tozo ambayo ni sahihi. Ninakushukuru.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU sliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo la uhaba wa Hosteli kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu wanaosoma katika Vyuo vya Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kutumia utaratibu wa ubia na sekta binafsi katika kujenga mabweni kwenye Vyuo na hata kwenye Sekondari?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Kimei kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Kimei ametoa wazo, naomba tulichukue ushauri wake tuende tukaufanyie kazi ili tuweze kuangalia ni nimna gani tunaweza tukajenga hosteli kwa njia ya PPP. Ninakushukuru.